*************************************
Na Mwandishi wetu, Hanang’
Matukio Mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Siku ya wanawake Duniani Yaliyofanyika Kimkoa Katika Kata ya Basutu Wilayani Hanang.
Maadhimisho hayo yameongozwa na kauli mbiu isemayo..
*Wanawake katika Uongozi Chachu kufikia Dunia yenye Usawa*
Akihutubia katika Maadhimisho hayo Mkuu wa
wilaya ya Hanang Ndugu *Ghaibu Lingo* kwa Niaba ya Mgeni Rasmi ambae ni
Mkuu wa Mkoa wa Manyara amewapongeza Wanawake Wote wa Mkoa wa Manyara
kwa Jinsi ambavyo wameendelea kushika nafasi kubwa za maamuzi na hivo
kuwepo kwa usawa miongoni mwa Jamii zetu kama ambavyo serikali yetu
inatutaka.
“Hapa Hanang tunae Mwenyekiti wa Halmashauri
ambae ni Mwanamke Mh Rose kamili, hivo hatuna shaka kwamba kwenye nafasi
za uongozi tumeonyesha mfano mzuri na sasa ni jukumu lenu kina mama
mliopata nafasi hizo na wengine wote kuhakikisha mnazitumia vema kwa
manufaa ya jamii zetu na Taifa kwa kwa Ujumla” alisema Ndugu Lingo.
Kupitia Maadhimisho hayo Wanawake wa Mkoa wa
Manyara wakiongozwa na Mbunge wa Viti Maalum Mh Regina Ndege walitoa
zawadi ya Shuka kwaajili ya Vitanda vya Wagonjwa katika kituo cha Afya
Basutu.
Semina mbalimbali za Ujasiriamali, Afya na
Elimu ya Mazingira nazo hazikuachwa nyuma ambapo semina hizo zimelenga
zaidi kuwavusha kutoka hatua moja na kwenda hatua nyingine zaidi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...