Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi,
Mhandisi Dkt. Leonard Chamuriho akikagua mradi wa ujenzi wa barabara ya
Kibondo hadi Kabingo (km 62.5), inayojengwa kwa kiwango cha lami na
Kampuni ya China Henan International Cooperation kwa gharama ya Shilingi
Bilioni 80.9. Kushoto kwa Waziri ni Meneja wa Wakala wa Barabara
(TANROADS) mkoa wa Kigoma, Mhandisi Narcis Choma, anae elekeza ni
Mhandisi Mshauri Hamis Khatibu.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Dkt. Leonard Chamuriho akiangalia mpango kazi wa ujenzi wa barabara ya Kibondo hadi Nyakanazi (km50), inayojengwa kwa kiwango cha lami na Kampuni ya Nyanza Road Works Limited kwa gharama ya Shilingi Bilioni 45.9, bila VAT. Anae elezea mpango kazi huo ni Mhandisi Mshauri Sharma, alieushika ni Meneja wa Wakala wa Barabara mkoa wa Kigoma Mhandisi Narcis Choma.
Ujenzi wa Daraja la Mwiyovozi katika barabara ya Nyakanazi Kibondo (km 50), inayojengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi Bilioni 45.9 bila VAT. Mradi huo unafadhiliwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi mahiri wa Rais, Dkt. John Magufuli.
Bi. Christina Richard mtaalamu wa kupima udongo katika maabara ya kampuni ya China Henan International Cooperation (CHICO), inayojenga barabara ya Nduta-Kibondo-Kabingo (km 62.5), mkoa wa Kigoma kwa gharama ya shilingi Bilioni 89.9.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Dkt. Leonard Chamuriho akishuka kutoka kwenye kivuko cha MV. Mwanza upande wa Kigongo (Wilaya ya Misungwi), baada ya kukamilisha ziara yake ya kukagua miradi ya ujenzi wa barabara kutoka Kasulu (kigoma) hadi Nyakanazi (Kagera).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...