Na Amiri Kilagalila, Njombe 
Muungano
 wa wakulima wa zao la chai kupitia vyama vya ushirika MVYULU tarafa ya 
Lupembe mkoani Njombe wamekubaliana kusitisha mgomo wa uchumaji wa 
majani ya chai uliodumu kwa mwezi mmoja na kukubaliana kurejea shambani 
hapo kesho April 12 mara baada ya makubaliano ya ulipwaji wa madeni yao 
zaidi ya Bil 1 kutoka kwa wawekezaji wa viwanda vya Ikanga na Igombola. 
Mbunge
 wa jimbo la Lupembe Edwin Swale amesema uamuzi huo umefikia mara baada 
ya majadiliano kadhaa ikiwamo vikao vya mara kwa mara yaliokuwa 
yakifanywa baina ya serikali,wakulima,uongozi wa vyama vya ushirika 
pamoja na wawekezaji wa viwanda hivyo vya Ikanga na kiwanda cha Chai 
Lupembe (Igombola) 
“Tumefanya uamuzi huo mkubwa tukiwa 
tumekubaliana kwamba kuanzia sasa hatutasubiri wakulima kukaa zaidi ya 
miezi miwili bila kulipwa tena,kwa hiyo kwenye ahadi na wawekezaji wa 
Ikanga fedha ambazo wameahida kuwalipa wakulima wa chai mpaka mwishoni 
mwa mwezi 4, basi tarehe 15 mwezi wa 5 tunakutana kuthibitisha”alisema 
Edwin Swale 
Amesema mgomo wa kuchuma chai ulianza March mbili 
kutokana na malalamiko ya wakulima hao kuto kulipwa stahiki zao ili 
waweze kujikimu katika maisha 
“Tulifanya uamuzi huo tarehe mbili
 mwezi wa tatu kwamba wananchi wa tarafa ya Lupembe,tusitishe kuchuma 
chai na tuzungumze kwanza kuhusu malipo,wakati tunafanya uamuzi ule 
tulikuwa na madai ya miezi mitano ya kulipwa,na mpaka hivi 
ninavyozungumza mwekezaji wa Ikanga amelipa fedha ya miezi 5 na anadaiwa
 mwezi wa pili tu” aliongeza Edwin Swale Mbunge wa Lupembe 
Ameahidi
 kuzungumza na waewekezaji ili kuweka utaratibu mzuri wa ulipwaji wa 
fedha za wakulima“Tunataka tuweke utaratibu mzuri ni lazima wakulima wa 
chai walipwe kila mwishoni mwa mwezi fedha yao wanayostahili kulipwa na 
niwahakikishie wananchi hii ndio kazi mliyonituma,niwahakikishie madai 
ya mwezi wa pili yatalipwa na madai ya mwaka 2018 yatalipwa” Edwin Swale
 Mbunge wa Lupembe akiwa kwenye mkutano na wananchi wa Lupembe 
Vile
 vile amesema wawekezaji wa kiwanda cha Igombola mpaka sasa ndio 
waliobakiwa na madai ya muda mrefu ukilinganisha na madai yaliyopo kwa 
wawekezaji wengine kutokana na kupunguza madeni yao. 
“Wawekezaji
 wa Igombola hali yao ni mbaya zaidi,kwasababu kuanzia mwezi wa 12,1,2 
na 3 hawajawalipa fedha wakulima wa chai na ahadi waliyoitoa kwenye 
kikao mpaka tarehe 26 mwezi huu watakuwa wamewalipa wakulima malipo 
yote” Edwin Swale 
Hata hivyo amewataka wakulima wa chai kuto 
kukata tama na kilimo hicho na kuhamia katika kilimo kingine badala yake
 waweze kujihusisha na kilimo kingine pia ili kuwa na uwanja mpana wa 
kukuza vipato vyao 
 “Mlio kata tamaa ya kuchuma chai na kuamua 
kwenda kupanda parachichi na miti,nawaombeni mfanye mambo yote,kwasabbu 
unavyopanda parachichi na zenyewe zikawa nyingi,kuna siku soko 
litaanguka kwa hiyo msitupe chai.Wajibu wangu na viongozi wengine 
tutahakikisha wakulima mnalipwa kwa wakati” alisema Swale 
Kutokana
 na hali hiyo wamiliki wa viwanda hivyo wamesema kutokana na kufikia 
makubaliano hayo pia ikiwemo kuchuma majani safi na yenye viwango 
stahiki wapo tayari kukamilisha malipo kabla ya mwezi Mei huku wakulima 
wakikubaliana kukutana Mei 15 ili kujadili utekelezaji wa makubaliano 
hayo.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...