Charles James, Michuzi TV

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora, Mohammed Mchengerwa amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuacha kutumia vibaya mamlaka zao kuwaweka ndani kinyume na sheria watu wanaotenda makosa huku akiwataka kuzingatia Utawala wa haki na sheria.

Hayo ameyasema jijini Dodoma wakati akizungumza na watumishi wa Wizara yake ikiwa ni siku kadhaa tangu ateuliwe na Rais Suluhu Hassan kushika nafasi hiyo akichukua nafasi ya Kepteni George Mkuchika ambaye ameteuliwa kuwa Waziri asiye na wizara.

Akizungumza katika kikao hiko, Mchengerwa amesema Wakuu wengi wa Mikoa na Wilaya wamekua wakitumia vibaya mamlaka yao waliyopewa kikatiba ya kuwaweka ndani masaa 24 hadi 48 watu waliofanya makosa huku akisisitiza viongozi hao kutambua kuwa Serikali ya Rais Samia inazingatia haki na utawala bora.

Waziri Mchengerwa pia ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa kuondoa kesi zote zilizopo mahakamani ambazo wanaona kwamba serikali haina uelekeo wa kushinda.

" Kumekua na mfulululizo wa kesi nyingi ambazo TAKUKURU inazipeleka mahakamani lakini haina ushahidi wa kutosha, niwaombe kuziondoa kesi zote ambazo hatuna uhakika wa kushinda, ni kupoteza fedha na muda kuendesha kesi ambazo mwisho wake wenyewe tunaona hatutoshinda.

Maelekezo mengine ni kwamba TAKUKURU iharakishe uchunguzi ambao Rais Samia aliagiza ufanyike kwenye Mamlaka ya Bandari nchini TPA, lakini pia iongeze juhudi za haraka kufikisha kesi za rushwa mahakamani kwa sababu hakuna kesi nyingi zilizopelekwa mahakamani badala yake kumekuepo na majadiliano nje ya mahakama," Amesema Mchengerwa.

Ametoa pia onyo kwa maafisa utumishi wote nchini kuhakikisha wanasimamia na kutatua changamoto za watumishi nchi na yeyote ambaye atashindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo hatosita kumuagiza Katibu Mkuu Utumishi kumuondoa kwenye nafasi hiyo.

" Haiwezekani watumishi wapate changamoto kwenye nafasi zao halafu kuna Maafisa Utumishi, niwatake maafisa utumishi wote kushughulika na changamoto za watumishi nchini na atakayeshindwa tutamuondoa kwenye nafasi hiyo," Amesema Mchengerwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...