TAASISI ya FURAHIKA Education College imetoa vifaa vya michezo  vyenye thamani ya shilingi laki 6 ikijumuisha jezi, mipira na trucksuit huku lengo kuu ikiwa ni  ni sehemu ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali hasa kwa kutoa elimu bure na kuboresha sekta ya michezo mashuleni.

Akizungumza na waandishi wa habari  leo Ilala jijini Dar es Salaam mratibu wa miradi ya michezo kwa watoto mashuleni kwa ngazi ya Wilaya na Mkoa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Furahika Education College, David Msuya amesema, katika maandalizi ya michezo ya UMISETA na UMITASHUMTA taasisi hiyo imetoa jezi, mipira na tracksuit kwa ajili ya maafisa wa michezo kwa wilaya za Kigamboni, Ubungo na jiji la Ilala ili ziweze kushiriki na kushinda katika mashindano hayo.

Msuya amesema, taasisi hiyo imekua ikishiriki katika uboreshaji wa elimu pamoja michezo mashuleni katika kuwajenga wanafunzi na amewashauri wadau wengine kuunga mkono jitihada hizo kwa kutoa vifaa na kushiriki kukarabati maeneo ya michezo vikiwemo viwanja.

Kwa upande wake mratibu wa michezo Mkoa wa Dar es Salaam Adolf Ally amesema, vifaa hivyo vitaleta tija mashuleni na kuwaomba wadau wengine kuisaidia Serikali inayotoa elimu burekwa  kuisaidia sekta ya michezo mashuleni kwa  kutatua changamoto ya viwanja vya michezo na  na vifaa.








Mratibu wa miradi ya michezo kwa watoto mashuleni kwa ngazi ya Wilaya na Mkoa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Furahika Education College David Msuya (Kulia,) akikabidhi vifaa vya michezo kwa mratibu wa michezo Mkoa wa Dar es Salaam Adolf Ally (kushoto,)ambavyo vitawasaidia wanafunzi watakaoshiriki mashindano tajwa kwa Wilaya za Ubungo, Kigamboni na Jiji la Ilala.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...