NAIBU
Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kagahe amewataka wajasiriamali
nchini kuzalisha bidhaa zenye ubora ili ziweze kuhimili ushindani wa
masoko ya ndani na nje ya nchi.
Naibu
Waziri Kagahe, ameyasema hayo juzi mjini Babati mkoani Manyara, kwenye
ufunguzi wa maonyesho ya 16 ya kanda ya kaskazini ya shirika la
kuhudumia viwanda vidogo nchini Sido.
Amesema
umuhimu wa kuzalisha bidhaa zenye ubora, utasababisha zipate soko ndani
na nje ya nchi hivyo wajasiriamali wa Tanzania wazingatie hilo.
Pia,
amesema katika kuhakikisha lengo la kukuza uchumi wa viwanda linatimia,
serikali inaendelea kubuni sera na mikakati ya kukuza uwekezaji kupitia
wajasiriamali wadogo.
"Serikali
inaandaa sera mpya ya maendeleo ya viwanda vidogo na biashara ndogo
ambayo pamoja na mambo mengine imetazama namna bora ya kuwawezesha
wajasiriamali vijana kuingia katika shughuli za kiuchumi," amesema.
Amesema
serikali inaendelea na hatua mbalimbali za kuwawezesha wajasiriamali
wadogo, wa kati na wakubwa katika kukuza fursa za masoko kwa kuendelea
kupanua wigo mpana wa masoko katika jumuiya ya Afrika Mashariki,nchi za
SADC, ambapo pia kwa sasa serikali ipo katika hatua za mwisho kulipia
mkataba wa eneo huru la biashara Afrika.
Amewataka wajasiriamali kutumia masoko hayo kikamilifu ili serikali ipate nguvu ya kuendelea kuwatafutia fursa zaidi.
Amesema
sekta ya Viwanda na Biashara nchini imeendelea kuongeza miundombinu ya
kufanyia kazi wajasiriamali wadogo katika mitaa ya viwanda vidogo vya
Sido ambapo mpaka sasa imejenga zaidi ya majengo 15 kwenye mikoa ya
Manyara, Geita, Kigoma, Mtwara na Dodoma kwa ajili ya uzalishaji, kazi
hiyo ni endelevu.
Mkurugenzi
mkuu wa Taasisi ya TEMDO iliyo chini ya wizara ya Viwanda na Biashara
inayohusika na utafiti, usanifu na utengenezaji wa Teknolojia mbalimbali
mhandisi Profesa Fredrick Kahimba, amewataka wenye changamoto ya
teknolojia kuwasiliana nao ili kupata msaada na biashara zao kupata
tija.
Amesema katika kuwafikia wajasiriamali wadogo wanawatembelea katika mikoa mbalimbali na kupitia mtandao wa Sido.
Maonesho
hayo ya 16 ya Sido yanabebwa na kauli mbiu isemayo Maendeleo ya
viwanda nuru ya maendeleo kiuchumi, yanatarajiwa kufungwa Mei 31,2021 na
mkuu wa mkoa wa Manyara Charles Makongoro Nyerere.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...