Na Victoria Robert,Geita.

Mkuu wa mkoa wa Geita Rosemary Swenyamule ameanza kazi rasmi kwa kutoa maagizo kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya mji Geita kwa kumtaka kuziboresha/kuzikarabati,standi ya mabasi yaendayo mikoa na wilaya mbalimbali pamoja na ile ya magari madogo,kwani standi hizo haziendani na mkoa uliobarikiwa rasilimali nyingi ikiwemo dhahabu ambayo inazaliwa asilimia 40, na kuufanya mkoa huo kuwa wa kwanza kwa uzalishaji dhahabu nchini.

Maagizo hayo ameyatoa wakati wa makabidhiano ya ofisi kati ya aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Geita  Mhandisi Robert Gabriel ambae ameamishiwa mkoa wa Mara ambapo amehaidi kutekeleza miradi yote ya maendeleo  ambayo ilianzishwa na mhandisi Gabriel ili kuwaletea maendeleo wananchi wa Geita.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...