Na Mwandishi wetu

CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) kimempongeza Katibu Mkuu wa Chama hicho Daniel Chongolo kwa kuanza kutoa mwelekeo na dira ya majukumu ya sekretariet ya NEC kwa muktadha kuisimamia na kufuatilia utendaji wa Serikali utakoleta tija na manufaa kwa umma.

Hivyo sekreterieti ya NEC  haitakuwa tayari kuona watanzania wakihangaika ,kutahabika na kukosa aidha haki za msingi, au wakifanyiwa dhuruma na udhalilishaji wa aina yoyote.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi( CCM) Shaka Hamdu Shaka wakati akikabidhiwa ofisi rasm na aliyekuwa mtangulizi wake Humphrey Polepole.

Shaka amesema  ni kawaida yanapotokea mabadiliko wahusika kukabidhiana kazi za kiofisi na kuongeza kama kazi ya utendaji  za CCM , Katibu Mkuu Daniel Chongolo ni kama upele ulimpata mkunaji kutoka na upeo alionao kisiasa na kiutendaji

Amesema atakuwa  tayari kutoa kila alichonacho kusaidiana na wenzake lakini pia atakuwa tayari kupokea na kujifunza kutoka kwa wenzake akichukua na kupokea mawazo, ushauri, miongozo na kuwa mjasiri  wa kusimamia changamoto chini ya shabaha na  malengo ya CCM

Aidha amezitaka taasisi  za umma na za kiserikali kila moja kutimiza wajibu wake kwa kutumikia  na kufuata miongozi ya kisera na malengo ya kimkakati yalioainishwa kwenye Ilani ya uchaguzi ya CCM  ya mwaka 2015/2020.

"Wote ni mashahidi   Rais Samia Suluhu Hassan  amechukua  jitihada za  wazi za kujenga mahusiano yanayochochea msukumo wa  biashara na uwekezaji,ameondoa vizuizi vya kibiashara kwa manufaa ya wote na amewahimiza wafanyabiashara na wananchi kulipa kodi,kodi isiwe bughudha na kizuizi bali kila mmoja alipe kwa wakati na hiari,"amesema Shaka.

Ameongeza Rais Samia ana nia ya dhati na kweli amedhamiria kujenga nchi huku akitaka iende kwa mwendo wa haraka ndio maana ameanza kufungua milango iliotaka kujifunga akifuata nyayo za watangulizi wake ambao wote  walipikwa, kuandaliwa na kupewa dhamana uongozi na CCM.

"Kwa dhamana nilionayo naahidi kuwa kiungo na daraja kwa watendaji wenzangu na makundi ya wanahabari, wanamichezo, wasanii na walemavu .Rais samia ameshasema upepo uwe mwingi au kidogo jahazi litatia nanga katika bandari ya mafanikio. CCM pia inaunga mkono msimamo huo na kutekeleza kwa vitendo" amesisitiza .

Pia Shaka amewasihi  viongozi wa taasisi za Serikali , mamlaka ,wakala mbalimbali za serikali na kujitafakari ili kuona muhimu qa  kumuunga mkono Rais Samia kwa utendaju wenye tija hatimaye wananchi wanufaike na  kufikia kilele cha maendeleo ya  kiuchumi, kijamii na kisiasa .

Akizungumzia kukabidhiwa ofisi, Shaka amemshukuru Polepole kwa kazi aliyoifanya yeye na wenzake wote huku akiahidi kuacha  wazi milango ya idara hiyo kwa namna yoyote ile ya kupokea ushauri kwa maslahi ya CCM na maendeleo   Taifa

"Katibu Mkuu wetu amekusudia kuwa na Chama linachotegemewa na wananchi nyakati  zote. CCM hakijawahi kuwa Chama cha masetla hivyo kitaendelea kubaki ni  chama cha wakulima na wafanyakzi chenye nia ya kujenga jamii ilio sawa na huru,"amesema Shaka.







 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...