Charles James, Michuzi TV

SPIKA wa Bunge, Job Ndugai amewaapisha wabunge wawili wapya kutoka mkoani Kigoma ambao ni Dk Florence Samizi wa Jimbo la Muhambwe na Kavejuru Felix wa Jimbo la Buhigwe wote wanatokana na Chama Cha Mapinduzi CCM.

Wabunge hao wamechaguliwa kuwa wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mdogo uliofanyika katika majimbo hayo Mei 16 mwaka huu.

Dk Florence Samizi wa Jimbo la Muhambwe amechaguliwa kufutia kifo cha aliyekua Mbunge wa Jimbo hilo, Mhandisi Atashasta Nditiye ambaye alifariki Dunia kwa ajali ya gari akiwa jijini Dodoma.

Kwa upande wake Mbunge wa Buhigwe, Kavejuru Felix amechaguliwa kuwa Mbunge kufuatia aliyekua Mbunge wa Jimbo hilo, Dk Philip Mpango kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
SPIKA wa Bunge, Job Ndugai akimuapisha Dk Florence Samizi wa Jimbo la Muhambwe
SPIKA wa Bunge, Job Ndugai akimuapisha Mbunge wa jimbo la Buhigwe, Kavejuru Felix



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...