Na Leylah Nassib - DSJ 

MTANGAZAJI  wa kipindi cha Mashamsham kinachorushwa Wasafi FM, Khadija Isihaka Shaibu maarufu kama Didah jioni ya jana amefunga ndoa na Diwani wa  Vingunguti na Meya wa Jiji la Dar es Salaam Omary Kumbilamoto.

Ndoa hiyo imekuja baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu kufuatia na mbwembwe nyingi za baadhi ya wasanii na wafanyabiashara kuahidi pesa ndefu za kutoa katika harusi hiyo ambapo wasanii na waigizaji wakiwemo Diamond platnumz, Rayvanny, Mbosso, Irene Uwoya, Aunt Ezekiel na wengine wengi walihaidi kutoa pesa nyingi ili kufanikisha shughuli hiyo.

 Ndoa hiyo ilifanyika Sinza nyumbani kwa akina Didah, na kupitia ukurasa wake wa Instagram Didah ameweka video na kuchapisha ujumbe ujumbe wa kuthibitisha tayari amekuwa mke wa mtu na ametoa shukurani zake za dhati kwa Mama Diamond 'Mama dangote' na Mumewe Uncle Shamte pamoja na Dada wa diamond Esma platnumz pamoja na watangazaji wenzake wa Wasafi Media na kuwaalika kuhudhuria sherehe zaidi ya ndoa hiyo leo katika ukumbi wa Escape One. 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...