Mjumbe wa kamati ya Miss Maendeleo Diana Willium akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mashindano hayo ambapo amewataka mabinti kutumia fursa hiyo adhimu ili kuweza kujijenga wao binafsi na jamii kwa ujumla, leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa kamati ya Miss Maendeleo Moses Soud akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamasha la Miss Maendeleo litakalofanyika katika Mikoa mitatu ya Dar es Salaam, Manyara na Dodoma leo jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa kamati ya Miss Maendeleo Madina Mjata maarufu kama Zawadi akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamasha la Miss Maendeleo  na kusema kuwa  mashindano hayo yatakuwa wa tofauti hivyo wazazi wasisite kuwaruhusu mabinti kushiriki, Leo jijini Dar es Salaam.


 

MABINTI kutoka mikoa mitatu ya Dar es Salaam, Dodoma na Manyara wamepata fursa ya kunadi shughuli zaa maendeleo ya Serikali na jamii kupitia shindano la 'Miss Maendeleo' linalotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mkoani Dar es Salaam Mwenyekiti wa shindano hilo Moses Soud amesema, shindano hilo la kwanza kufanyika limelenga kuwainua mabinti ambao pia watakuwa mabalozi wa kutangaza shughuli za maendeleo zinazofanywa na Serikali na jamii kwa ujumla.

Amesema, shindano hilo litakalofanyika katika mikoa mitatu litahusisha mabinti wenye elimu kuanzia kidato cha nne, wenye akili timamu, watanzania wanaozungumza lugha mbili na zaidi na wenye umri kuanzia miaka 18-25 na baada ya  washindi kutoka katika Mkoa kupatikana watachuana kumpata mshindi wa jumla na zawadi nono zitatolewa.

Amesema fomu za ushiriki zinapatikana katika chama cha waigizaji Ilala na Chuo cha Furahika Education College kilichopo Buguruni Malapa na tayari Wizara husika na baraza la sanaa la Taifa (BASATA,) wamebariki mashindano hayo.

Kwa upande wake mjumbe wa kamati ya mashindano hayo na mwigizaji wa filamu Diana William amesema hiyo ni fursa kwa mabinti ambayo itawasaidia kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii pamoja na kuibua vipaji vyao na amewashauri wazazi kuwaruhusu mabinti kushiriki katika mashindano hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...