MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam  Amos Makalla leo amefanya kikao cha pamoja na Maafisa Afya na Mazingira kutoka Wilaya tano za Mkoa huo kwa lengo la kujadiliana hatua za mwisho za ukamilishaji wa Mpango Mkakati wa kuifanya Dar es salaam kuwa Safi.

Katika kikao hicho RC Makalla alitaka kujua ni mambo gani yamekuwa kikwazo kwao hadi kusababisha Jiji kuwa Katika hali ya uchafu na nini kifanyike ili kampeni ya usafi inayopangwa kuanza hivi karibuni iweze kuwa na mafanikio makubwa.

RC Makalla amesema lengo lake ni kuona Dar es salaam inakuwa katika hali ya usafi kwakuwa Jiji hilo linabeba taswira ya Nchi na ndilo linalopokea wageni wa mataifa mbalimbali hivyo ni lazima liwe kwenye hali ya usafi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...