Kipekee familia inatoa shukurani kwa madaktari na wauguzi katika hospitali ya Wilaya ya Rungwe, Makandana mjini Tukuyu, Hospitali ya Rufaa ya Mbeya na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, hususan kitengo cha dharura chini ya Dkt Juma Mfinanga na Dkt Suphiani, kwa kujitoa kwa moyo wote kujaribu kuokoa maisha ya mpendwa wetu.
Salaam hizi pia ziwafikie uongozi wa Chai FM kwa kujitoa ka hali na mali wakati wa kuugua na hatimaye kifo cha ndugu yetu.
Ni vigumu kumtaja na kumshukuru kila mmoja wenu kwani ni wengi mno. Hivyo itoshe tu kusema familia hii inawashukuruni sana sana kwa moyo wa upendo mliounesha kwetu. Hatuna cha kuwalipa ila ni Mola pekee atayewalipa.
ASANTENI SANA NA MBARIKIWE.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...