WAGANGA  wa Jadi wa Wilaya ya Itilima wameungana na kujenga madarasa mawili katika shule ya Sekondari Chinamili. 

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu David Kafulila amewapongeza Waganga hao wa Jadi kwa mchango wao mkubwa wa maendeleo katika sekta ya elimu kwa kujenga  madarasa hayo. 

Kafulila amesema ujenzi wa madarasa hayo mawili  umeonyesha uthamini wa waganga hao wa jadi katika elimu, na kuondoa dhana ya kwamba  waganga wa jadi hawathamini elimu.Hali kadhalika wameunga mkono jitihada za Serikali katika masuala ya elimu.

Vilevile ameeleza kufurahishwa sana na jitihada hizo na kuwataka kutosita kumshirikisha k pindi wanapohitaji msaada na amewaunga mkono kwa kutoa milango miwili ya vyumba vya madarasa hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...