Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu David Kafulila amewapongeza Waganga hao wa Jadi kwa mchango wao mkubwa wa maendeleo katika sekta ya elimu kwa kujenga madarasa hayo.
Kafulila amesema ujenzi wa madarasa hayo mawili umeonyesha uthamini wa waganga hao wa jadi katika elimu, na kuondoa dhana ya kwamba waganga wa jadi hawathamini elimu.Hali kadhalika wameunga mkono jitihada za Serikali katika masuala ya elimu.
Vilevile ameeleza kufurahishwa sana na jitihada hizo na kuwataka kutosita kumshirikisha k pindi wanapohitaji msaada na amewaunga mkono kwa kutoa milango miwili ya vyumba vya madarasa hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...