NA YEREMIAS NGERANGERA…NAMTUMBO.

Mbunge wa  jimbo la Namtumbo Mheshimiwa Vitta Rashidi Kawawa ameyasema hayo katika kikao alichokifanya na wakuu wa idara na vitengo katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo kuwa wakulima hawajalalamikia mfumo wa kuuza kwa njia ya stakabadhi ghalani kwa maana hiyo mfumo huo  ni mzuri na unafaa kwa wananchi wa wilaya ya Namtumbo.

Kawawa alidai ameanza ziara ya kuzungumza na wananchi wa jimbo lake kusikiliza kero  za wananchi lakini alisema katika vijiji alivyozungumza na wananchi inaonyesha wazi wakulima wanafurahishwa na kuuza mazao yao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.

Hata hivyo  Kawawa alisema wapo wafanyabiashara wadogo aliowaita kwa jina la wachuzi wanaonesha kutoridhika na mfumo huo kwa kuwa walikuwa wananufaika na mfumo holela wa kuuza mazao lakini aliwaomba wataalamu kusimamia mfumo huo wa kuuza mazao kwa njia ya stakabadhi ghalani kwa lengo la kuwasaidia wananchi waliowengi na wenye kipatao cha chini.

Afisa kilimo,Ushirika na umwagiliaji  wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Joseph Mbilinyi alimwambia Mbunge huyo kuwa wakulima wa wilaya ya Namtumbo wameuelewa mfumo wa stakabadhi ghalani lakini wanachodai mfumo huo uwekewe  bei elekezi  na serikali badala ya kuacha wafanyabiashara waamue bei  wenyewe hali  inayowatia hofu wakulima wa wilaya ya Namtumbo .

Bwana Mbilinyi aliongeza kuwa wananchi wanahoji wakati mfumo wa kuuza mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani umeanzishwa katika wil;aya ya Namtumbo serikali iliweka bei elekezi  na wafanyabiashara walinunua kwa bei ya juu ya ile iliyowekwa na serikali lakini serikali ilipoacha kuweka bei elekezi bei hazieleweki wanadai wakulima alisema bwana mbilinyi.

Mkurugenzi  wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Evance  Nachimbinya  kwa niaba ya watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo alimpongeza mbunge huyo kwa kufanya kikao na watumishi hao kwa lengo la kujenga ushirikiano  katika kutekeleza majukumu ya kuwahudumia wananchi wa Namtumbo.

Nachimbinya alimhakikishia mbunge kuwa  wataalamu wa Halmashauri na watumishi wote kwa ujumla wao watampa ushirikiano  wa hali na  mali Mbunge  huyo katika kuhakikisha shughuli za kuwahudumia wananchi wa Namtumbo zinafanikiwa kwa kiwango cha juu.

Jimbo la Namtumbo mkoa wa Ruvuma  chini ya mbunge  Vitta Rashid Kawawa lina jumla ya kata 21, tarafa 3, vijiji 66 na mamlaka ya miji midogo 2 na miji midogo 7 ambapo wananchi wake ni hodari katika kilimo cha mazao ya biashara na chakula huku ardhi yake ni yenye rutuba na inayofaa kwa kilimo.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...