Na Linda Shebby

MAMIA ya wakaazi wa Mkoa wa Dar Es Salaam leo walihudhuria tamasha  lililofana ambalo lilikwenda kwa jina la 'Mihogo Festival' lililofanyika kwenye ufukwe wa Coco, maarufu kwa jina la 'Coco Beach' ambako kumesheheni wachuuzi wa mihogo ya kukaanga na mishikaki.

Akizungumza na waandishi wa Habari  Mkurugenzi wa Ubunifu kutoka Clouds Media Group (CMG) Sebastian Ndege amesema imekuwa ni kawaida  kwao kuwa wabunifu  kwa kuleta michongo kwa jamii  ikiwa ni  katika kupandisha thamani ya kitu chochote Kama jinsi walivyoipandisha thaamani  mihogo chakula ambacho wapo baadhi ya watu  ambao wamekua wakiushusha thamani muhogo huku zao hili likiwa ni lenye thamani ulimwenguni.

"Ifike wakati sisi Watanzania tujivunie  asili yeti kama jinsi ambavyo mtu unaweza kwenda katika nchi za wenzetu  Kama Italy wao wana tamasha lao la Pizza Festival vivyo hivyo na sisi tumekuja na tamasha  hili la Muhogo Festival" Alisema Ndege.
Aidha tamasha Hilo lilinogeshwa na wasanii mbalimbali akiwemo msanii Mkongwe katika muziki  wa dansi Muumin Mwinjuma,Malaika, Bosho,Ferouz,Rich Mavoko,Kayumba,Fay Melody,Ney Wamitego, Msami,Sarafina,,Young D,Frida Amani, Country Boy,DJ ODG,Dulla Makabila na Sholo Mwamba.

Aidha Ndege aliongeza kwa kusema kuwa chachu ya kufanyika kwa tamasha hilo ilitoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group (CMG)  Joseph Kusaga ambaye  ni  mteja  mkubwa wa  wachuuzi hao wa mihogo ambapo waliwahi kumuuliza mbali ya kuwa yeye ni mteja wao mkubwa wa mihogo atawafanyia nini ambapo aliwaahidi kuwaandalia tamasha hivyo ametimiza ahadi yake, Alisema.
Aliongeza kwa kusema kuwa CMG wamekua wakipandisha thamani bidhaa mbalimbali ikiwemo mtu mmojammoja ama vikundi, Kama Tasnia za urembo, michezo Ndondo Cup, Malkia wa Nguvu, na wasanii katika nyanja zote.
Watangazaji wa Clouds Tv Dacota Delavida na Sakina Lyoka wakiwa Jukwaani kwenye tamasha la Mihogo Festival lililofanyika kwenye Ufukwe wa bahari ya Hindi almaarufu Kama.Coco Beach Jijini  Dar  Es  Salaam
MC Konata anyetamba na miondoko ya Singeli akitoa burudani  kwenye tamasha la Mihogo Festival lililofanyika kwenye Ufukwe wa bahari ya Hindi almaarufu Kama.Coco Beach Jijini  Dar  Es  Salaam


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...