Na Linda Shebby,Bagamoyo

MWENYEKITI wa Baraza la Ushindani nchini 'Fair Competition Tribunal' (FCT) Jaji Stephen  Murimi amesema kuwa asilimia ya kesi 90 zilizohusiana na masuala ya Ushindani wa kibiashara ziliamuliwa katika kipindi Cha 2019 na 2020.

 Jaji Murimi alisema hayo alipozungumza na waandishi wa Habari  katika semina elekezi ya simu tatu kwa Wajumbe wapya  wa Baraza Hilo  ambao wameteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

"Wajumbe hawa sita wapya wametoka  katika fani mbalimbali ambapo tumepata wanasheria wanne,Mchumi mmoja na Profesa mmoja hivyo tumekutana hapa ili niweze kuwaelekeza yote wanayopaswa kuyafanya ndani ya Baraza letu"alisema Jaji Mrimi.
 Akizungumza na Michuzi Blog Mjumbe mpya  Dkt. Onesmo Kyauke  Ali anamshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua hivyo ana ahidi kufanya kazi kwa ufanisi.

 Dkt. Hanifa Massawe ambaye ni mwanamke pekee kwenye Baraza Hilo amesema atafanya kazi yake kwa uadilifu.
Mafunzo hayo ya siku tatu  kwa Wajumbeyalifanyika Bagamoyo Mkoani Pwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...