Leo Julai 19,2021  Naibu Balozi wa Ujerumani  nchini Tanzania Dkt. Kathrin Steinbrenner amemtunuku Dkt. Karl-Heinz Köhler tuzo ya the order of Merit Cross on Ribbon ya  Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani katika makazi ya Balozi.

Taarifa iliyotolewa leo na Kitengo cha Mawasiliano cha Ubalozi huo imesema kuwa Mwishoni mwa mwaka  2010, Dkt. Karl-Heinz Köhler pamoja na Mratibu wa Shirikisho wa miradi ya shule za UNESCO Ujerumani, Heinz-Jürgen Rickert na Mratibu wa Kitaifa wa mtandao wa shule za UNESCO nchini Tanzania, Modester M.Mwinula, walianzisha “Tasisi ya  ujifunzaji wa utamaduni na ubunifu /Shule za mfano za Afrika”

Ambapo kwa kipindi chote Dkt. Köhler amekuwa ni Mkurugenzi Mkuu.”Shule ya Sekondari  Dunia Moja Kilimanjaro” iliyoanzishwa mwaka 2012 kama mradi wa jaribio na ilikuwa mradi wa shule ya Unesco ya kwanza nchini Tanzania yenye mwelekeo wa kimataifa.

Imesema kwamba Shule ya  Sekondari ya Dunia Moja Kilimanjaro iliyopo Kisangara ,takriban km 60 kusini mwa Moshi na mkoa wa Kilimanjaro, inaunganisha mifumo ya shule za Ujerumani na Tanzania, mbinu za kujifunza za kijerumani  na pia wanafunzi wanajifunza Kijerumani kama lugha ya pili ya kigeni baada ya Kingereza. Shule imesimama katika mtindo wa kisasa wa elimu inayosaidia watoto wa Kitanzania na vijana kuwa  na maisha ya kujitegemea.

Kutokana na jitihada za Dkt. Köhler “Shule ya Sekondari  Dunia Moja Kilimanjaro” kwa sasa ni mojawapo ya shule tatu za PASCH nchini Tanzania.PASCH inawakilisha “Shule: Washirika wa siku zijjazo” mpango wa kijerumani iliyozinduliwa  Februari mwaka 2008 na ofisi ya Shirikisho ya Mambo ya Nje ya Ujerumani lenye lengo la kuamsha hamu na shauku kwa vijana kujifunza Kijerumani na kutengeneza mtandao wa kimatifa  wa  shule ambapo mpaka sasa inajumuisha shule 200 duniani kote.

Dkt. Köhler ametoa mchango mkubwa kwa sifa ya Ujerumani katika nyanja ya elimu.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...