Na Humphrey Shao,Michuzi TV Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto .Prof. Abel Makubi, amezindua zoezi la usambazaji wa chanjo ya UVIKO 19 aina ya Jonson Jonson Kwenye BOHARI ya Dawa (MSD) iliyopo Keko Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Waandishi wa habari mara baada uzinduzi huo Prof .Makubi amesema chanjo hizo zitasambazwa katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara.
"Chanjo hizi ni Bure na zitapatikana katika Hospitali zote zitakazo elekezwa za Serikali na zile za Binafsi ambazo zitakuwa zimeteuliwa" Amesema Prof Makubi.
Amesisitiza kuwa chanjo hiyo ni Bure na Serikali imesambaza katika mikoa yote kwa idadi tofauti kulingana na visa vilivyoripotiwa katika mkoa huo.
Ametaja kuwa chanjo hii inaanza kutolewa kwa makundi maalum ambayo ni Wazee ,Watumishi , Watumishi wa majeshi na Wenye magonjwa hatarishi.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Dr.Benjamini Hubila amesema mchakato wa usambazaji umekamilika na shirika lake limejipanga vyema kupeleka chanjo hizo kwa wakati.
Amesema MSD itasambaza chanjo hizo ndani ya siku Saba kwa kupitia mtandao wake wa usambazaji dawa nchini
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Prof.Abel Makubi akikabidhi chanjo kwa Mkurugenzi wa MSD Dr.Benjamini Hubila.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Prof.Abel Makubi akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa usambazaji wa chanjo ya uviko 19 .
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MSD nchini, Dr.Benjamini Hubila akitoa ufafanuzi kwa Waandishi wa habari.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...