Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhe Abubakar Kunenge leo Agosti 11, 2021 majira ya saa 12 Asubuhi amepokea Mwenge huo kutoka kwa Mhe. Martine Shigela Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Kunenge Ameeleza kuwa Mwenge huo ukiwa Mkoani hapo utakimbizwa katika Wilaya saba za Mkoa huo na kufikia Miradi 87 ambapo Miradi 18 Itafunguliwa Miradi 9 Itawekwa mawe ya Msingi na Miradi 60 Itakaguliwa.
Miradi yote inathamani ya Shilingi 57,311,572,720. Ameeleza Miradi yote imezingatia Kauli Mbiu ya Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru 2021 Isemayo TEHAMA ni Msingi waTaifa Endelevu itumie kwa usahihi na Uwajibikaji.
Baada ya kupokea Mwenge huo Mhe Kunenge amekabidhi kwa Mhe Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Abdalah.
"Kwa niaba ya Wananchi wa Mkoa wa Pwani, ninayoheshima kubwa kuwakaribisha wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mkoani Pwani na kwa kipindi chote Mjiskie mpo Nyumbani kwa ndugu zenu wakarimu Wanapwani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...