Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
JESHI
 la polisi linamshikilia Antony Lugendo (34) mkulima,mkazi wa Mlandizi 
kwa kosa la kumdhalilisha mtoto mdogo wa kike miaka mitatu kwa kumchezea
 chezea sehemu za siri.
Aidha limekamata watuhumiwa 38 wa makosa mbalimbali na mali za wananchi zimeokolewa,ikiwemo TV,Radio,sabufa, pikipiki na laptop.
Akithibitisha
 kutokea kwa tukio Hilo,kamanda wa polisi mkoani Pwani ,Wankyo Nyigesa 
,alisema tukio limetokea juzi saa 10 jioni ,huko Kitongoji Cha Kaloleni 
kata ya Janga .
Alieleza
 ,mtuhumiwa alikamatwa akiwa chumbani kwake amemvua nguo zote na akiwa 
anamchezea mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa chekechea .
"Mtuhumiwa tumemkamata na upelelezi unaendelea ili hatua za kisheria zichukuliwe"alisema Wankyo.
Katika
 hatua nyingine, Wankyo alieleza kwa kipindi cha wiki mbili kuanzia 
septemba 3 hadi 17 septemba limefanya operesheni katika wilaya zake tano
 madhumuni kuzuia , kudhibiti uhalifu .
Katika
 operesheni hii walifanikiwa kukamata bunduki 1 aina ya shortgun yenye 
namba GP 719 na risasi moja ,bangi kwenye beg ,puli 39 ,kete 661 na 
miche 24,radio 2 aina ya sony na sabufa moja na spika 6 kati ya hizo 
aina ya boss 02 na aina ya sony nne.
Wankyo
 alifafanua ,pia laptop moja ,mafuta ya dizel lota 230 ,petrol lita 500 
,pikipiki moja aina ya boxer yenye namba za usajili MC 226 CMT rangi 
nyeusi na televisheni tano aina ya Good vision ,sony , Samsung,LG na TCL
 moja.
"Vitu
 vingine ni desktop moja aina ya dell na CPU mbili ,gari aina ya canter 
moja ,matairi mawili ya gari , camera mbili aina ya Samsung moja ,camera
 monitor,mkasi wa kukatia chuma ,funguo master key na pombe ya moshi 
lita 65.
Wankyo alikemea kwa jamii kuacha tabia ya unyanyasaji kwa watoto kwani kwa kufanya hivyo kuwaharibu kisaikolojia



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...