Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV

USHINDI walioupata Klabu ya Yanga wa bao 1-0 dhidi ya Klabu ya Simba na kuiwezesha klabu hiyo kutwaa Ngao ya Jamii umesababisha kifo cha askari H.2636 Rashid Mohamed Jumaa.

Askari huyo alikuwa akifanya kazi katika Kituo cha Polisi Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma na inaelezwa alifariki dunia saa 12 jioni alipokiwa akiangalia mtangane wa watani wa jadi Simba na Yanga maeneo ya Stendi ya basi ya Wilaya ya Mpwapwa.

Mtangane huo uliochezwa Uwanja wa Mkapa mkoani Dar es Salaam ulikuwa ukioneshwa Live na kituo cha Luninga cha Azam TV ambao ndio waliopewa jukumu la kuonesha mechi za Ligi Kuu nchini.

Wakati akishangalia na kuwa na furaha iliyopitiloza askari polisi huyo alianguka chini,hivyo alichukuliwa na kupelekwa Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa ambapo baada ya kufikishwa hapo madaktari walithibitisha alishafariki dunia.

Kwa mujibu wa taarifa inayoelezea tukio cha kifo cha askari huyo inadai alikuwa shabiki wa kutupwa wa Yanga na ushindi wa bao 1- 0 ambaoYanga waliupata katika dakika ya 11 ya mchezo huo uliochezwa jana Septemba 25 mwaka huu 2021 kuanzia saa 11 jioni ndio unaodaiwa kusababisha kifo hicho.

Askari huyo aliyekuwa akifanya kazi katika Wilaya ya Mpwampwa ni mwenyeji wa Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa.

 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...