Na  Linda Shebby ,Kibaha
WANAWAKE wa Mkoa  wa Pwani wamepewa  wito  wa kujitokeza kwa wingi  katika  kongamano  la Fursa Gala ambalo limepangwa kufanyika   Oktoba  3 mwaka huu kwenye ukumbi wa  Destiny uliopo Kwa Mathias Kibaha Mkoani Pwani

Akizungumza  katika mkutano na waandishi wa Habari Mkurugenzi wa  Kampuni ya Herochic ambayo ndiyo waandaaji Bi  Suzana Mdonya  alisema kuwa kongamano  hilo lina  lengo la kumkomboa mwanamke kiuchumi  ambapo pia wanatarajia kuwa litawakutanisha  wanawake kutoka katika Kanda  ya Pwani  na viunga vyake ikiwemo Mkuranga, Kibaha, Chalinze na Mlan na kuwawezesha  kujifunza  njia sahihi  za  biashara  na uwekezaji kutoka kw a  wakufunzi  mahiri nchini  na  kuwawezesha  wanawake  kuwa na nidhamu ya  mtaji wa biashara na fedha kwa ujumla ambazo wanazipata  katika kila  nyanja  ya ujasiriamali waoufanya.

"Tunakwenda  kumwezesha  mwanamke  Ili aweze  kutambua  thamani ya mtaji wake wa biashara na kumpatia  elimu na mbinu mbadala  ya kuweza kukuza mtaji wake  pamoja na kukua kibiashara  huku lengo likiwa  kumkomboa mwanamke kiuchumi" alisema Suzana

Aidha  kuwa kauli mbiu ya kongamano hilo ni ' Uwezo wa Mwanamke' ambapo pia katika  Fursa Gala  litawakutanisha  wajasiriamali wakubwa na wadogo, wamiliki wa Viwanda  huku lengo likiwa ni kupeana masoko ya biashara, kuongeza wigo wa kupata masoko kwa wajasiriamali.

Suzana  anakitaja kiingilio kwenye kongamano  hilo kuwa  ni 30,000 & 50,000 (VIP)
Akielezea kuhusu Herochic alisema kuwa  ni Kampuni binafsi  katika kutekeleza  majukumu ya kijamii  ambapo imeandaa kongamano hilo kwa kushirikiana na Vitenge  na Tamrah Kibaha,  HEROCHIC inayojishughulisha  na Ubunifu na ushonaji wa  sare za maofisi  pamoja na Suti za kiume na kike.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...