Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akikabidhiwa mavazi ya michezo kutoka kwa viongozi wa Shirikisho la michezo la mashirika ya umma na kampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo. Septemba 30,2021.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akikabidhiwa zawadi ya ngao ya heshima kutoka kwa viongozi wa Shirikisho la michezo la mashirika ya umma na kampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) akiwa mlezi wa shirikisho hilo mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo. Septemba 30,2021.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirikisho la michezo la mashirika ya umma na kampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo. Septemba 30,2021.

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango hii leo Septemba 30, 2021 amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma na Kampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA).

Katika mazungumzo hayo, Makamu wa Rais ametaja Michezo kama njia ya kuleta umoja na undugu katika maeneo ya kazi pamoja na kuondokana na maradhi mbalimbali. Amesema kupitia michezo ndio kunaweza pia kukabiliana na Uviko 19 pamoja na kutoa elimu ya kupata chanjo ya ugonjwa huo.

Makamu wa Rais ametoa rai kwa Shimmuta kutumia michezo wanayoisimamia kutoa elimu ya utunzaji mazingira. Amesema yapo maeneo mengi yanayohotaji upandaji miti pamoja na usafi wa mazingira hivyo Shimmuta inapaswa kuwa chachu ya kuhamasisha utunzaji wa mazingira kwa vitendo.

Aidha Makamu wa Rais ameiasa SHIMMUTA kufanya michezo itakayotoa mchango katika jamii kama vile Riadha zinazofanywa kwa lengo la kupata fedha na kusaidia katika huduma za kijamii.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Shimmuta, Hamis Mkanachi amesema changamoto inayoikabili Shimmuta ni ukosefu wa udhamini katika mashindano yanayoandaliwa pamoja ushiriki mdogo wa Mashirika, Kampuni na taasisi katika michezo hiyo.

Mashindano ya Shimmuta mwaka 2021 yanatarajiwa kufanyika mkoani Morogoro katikati ya mwezi Novemba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...