Na Khadija Kalili

JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani  kupitia Kamanda wa Mkoa RPC Wankyo Nyigesa ameanzisha  michuano ya  Kombe la Uhalifu Haulipi  2021  kwa lengo la kupunguza  vitendo vya Uhalifu ndani  ya Mkoa wa Pwani.

 RPC Wankyo alisema hayo leo  katika uzinduzi  wa michuano hiyo uliofanyika leo jioni katika viwanja vya Bwawani Kibaha Mkoani Pwani ambapo michuano hiyo itazishirikisha  timu za watu kutoka katika kada mbalimbali pamoja na timu  16.

Michuano imeandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kwa ushirikiano na  Chama Cha  Mpira  wa Miguu  Wilaya  ya  Kibaha (KIBAFA).

Alizitaja timu hizo ambazo zitashiriki katika michuano hiyo ni Bodaboda FC, Bwawani FC, Gereji, Hisia Kali FC, Juhudi FC, Kiswamba Electronicnics FC, Matunda FC, Mali Asili FC, Mlandizi Combine FC, Mailimoja FC, Wagosi FC, Wajeda FC, Wakulungwa FC, Tangini FC na Visiga FC.

Aidha RPC Wankyo alisema  kuwa michuano hiyo itafanyika ndani ya wiki mbili  huku timu hizo zikichuana katika mzunguko wa mtoano ambapo fainali itarindima  Oktoba 16  mwaka huu katika Uwanja wa Bwawani Kibaha.

Alizitaja zawadi zitakazotolewa ni ng'ombe  na kiasi cha  Sh. 100,0000kwa mshindi wa kwanza, mshindi wa pili atapata Mbuzi na kiasi Cha Sh. 100,000 watakaobaki watashikwa mkono.

Aidha aliyekuwa Mgeni rasmi katika uzinduzi wa michuano hiyo amewaagiza Jeshi la Polisi Kanda Maalumu  Kibiti  waanzishe  mashindano kama haya Ili waweze kuunda timu moja itakayo uwakilisha Mkoa.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...