Na Mwandishi Wetu, Ufaransa

UBALOZI  wa Tanzania nchini Ufaransa umefanya mkutano wa wadau wa utalii Ubalozini kwa madhumuni ya kuwahakikishia wadau hao utayari wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuendelea kupokea Watalii hususan kwa wakati huu baada ya dunia kukumbwa na janga la ugonjwa wa Corona  ambao umeathiri sana sekta ya utalii duniani kote.

Aidha,katika mkutano huo, uliofanyika Septemba 9,2021 Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Samwel Shelukindo alifahamisha wadau hao kuhusu juhudi zinazofanywa naSamia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambae ameamua kufanya ziara iitwayo "Royal Tour"katika maeneo makubwa yenye vivutio  nchini Tanzania.

Balozi Shelukindo aliwaeleza wadau kwamba jitihada hizo zinalenga kuitangaza Tanzania upya (Rebranding) na vivutio vyake vya utalii. Takriban wadau 60 walishiriki mkutano huo ambapo miongoni mwao ni makampuni makubwa yanayojihusisha na utalii (Tour Operators), Waandishi wa habari wanaotangaza utalii, Wafanyabiashara.

Wakati huo huo, Ubalozi unaratibu ziara ya kundi la Watalii 77 wanaotegemea kwenda Tanzania kuanzia tarehe 7 mpaka 12 Oktoba 2021 kutembelea maeneo mbalimbali.

Sehemu ya wadau wa utalii nchini Ufaransa wakimsikiliza Balozi wa Tanzania nchini humo Samuel  Shelukindo wakati akielezea utayari wa Serikali ya Tanzania kupokea watalii

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...