Benki ya CRDB yaingia mkataba na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) wa ujenzi wa jengo la kisasa la kutolea huduma katika lango kuu la chuo hicho.
Jengo hilo (mchoro pichani) ambalo linatarajiwa kugharimu shilingi milioni 150, litakuwa kituo cha huduma za kisasa za Benki ya CRDB, ATMs na skrini za kielektoniki zitakazokuwa na matangazo ya huduma zitolewazo na benki pamoja na huduma za kujihudumia (Self Service).
Huduma nyingine zitakazotolewa ni pamoja na zile za Chuo Kikuu cha Dodoma kama za usalama, maelekezo kwa wageni wa chuo, na banda la ulinzi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...