Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB) Godfred Mbanyi amefunga Semina ya 23 'Research Workshop'  iliyokuwa na lengo la kutoa mafunzo maalumu ya kuwandaa  wanafunzi wa Bodi wanaotarajiwa kufanya tafiti kabla ya kuhitimu mafunzo kutoka bodi hiyo yaliyoanza  Sepitemba 27 hadi leo Oktoba 01, 2021.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo Godfrey Mbanyi amesema wanafunzi wa Bodi wanapaswa kuwa waaminifu kwenye sehemu za kazi ili serikali iweze kupata kodi stahiki ili kufikia malengo yaliyowekwa hasa kuhudumia wananchi.

Mbanyi amesema, serikali iko macho na hatua stahiki zitachukuliwa kwa wale wanaokiuka maadali ya Taaluma ya Ununuzi na Ugavi. Pia amesisitiza wale anaokuwa wazoefu kazini inahitaji sana kuwalea wafanyakazi wachanga au waajiliwa wapya  wawe na maadili mazuri hasa kwenye kufanya kazi za manunuzi.

Aidha amewakemea vikali  watu ambao ni wazoefu kazini kuwaelekeza waajiliwa wapya kwenye maeneo ya kazi taratibu na njia mbaya zinazokiuka mienendo  na maadili ya taaluma ya ununuzi na ugavi.

Pia amesema hii itaweza kusaidia kutoa huduma nzuri kwa wananchi na kuondoa lawama ambazo zinaweza kutolewa kwa Serikali. Na Serikali pia inaweza kulaumiwa na matendo ambayo yanatendwa na watendaji ambao wameaminiwa kuweza kufanya kazi kwa niaba ya hao wananchi.

Leo baada ya kuhitimu mafunzo ya siku tano wahitimu wamepewa vyeti vya kuonesha ushiriki wao katika mafunzo hayo ili kuanza kuandika research proposal/ mapendekezo ya tafiti zenu mapema iwezekanavyo.

Wanafunzi wa Bodi wapatao 134 wameshiriki mafunzo maalumu ya kuwandaa  wanafunzi wa Bodi wanaotarajiwa kufanya tafiti kabla ya kuhitimu mafunzo yaliyoandaliwa na Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB).


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB), Godfred Mbanyi akizungumza wakati wa kufunga semina ya 23 'Research Workshop' iliyokuwa na lengo la kutoa mafunzo maalumu ya kuwandaa wanafunzi wa Bodi wanaotarajiwa kufanya tafiti kabla ya kuhitimu mafunzo kutoka bodi hiyo yaliyoanza toka Sepitemba 27 hadi leo Oktoba 01, 2021 katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini  Dar es Salaam leo.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB), Godfred Mbanyi akiwakabidhi baadhi ya wanafunzi wa Bodi walioudhulia semina ya 23 'Research Workshop' iliyokuwa na lengo la kutoa mafunzo maalumu ya kuwandaa wanafunzi wa Bodi wanaotarajiwa kufanya tafiti kabla ya kuhitimu mafunzo kutoka bodi hiyo.
Baadhi ya wanafunzi wa Bodi wanaotarajiwa kufanya tafiti wakifuatilia hotubaya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB), Godfred Mbanyi alipokuwa anafunga mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku tano yaliyoanza toka Sepitemba 27 hadi leo Oktoba 01, 2021 katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...