Na Khadija Kalili 
Mkurugenzi wa Chuo Cha Afya na Sayansi Shirikishi (City College of Health and Allied Sciences) Shaban Mwanga ametoa wito kwa wanafunzi wa  Chuo hicho na jamii  kuchangia damu Ili kusaidia  Kituo Cha Afya Cha mama na mtoto iliyopo Chanika Ilala Dar es Salaam.
Mkurugenzi huyo alisema hayo leo alipokuwa  akiongoza zoezi la kuchangia  damu   lilofanyika kwenye viwanja vya  Chuo hicho ikiwa ni katika kilele cha kutimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa tawi la hilo  la Chanika.

" Nawahamasisha  wakaazi wote wa Chanika , wanafunzi wa Chuo changu wajitokeze kwa wingi katika kuchangia damu  kwa sababu  itasaidia kuokoa maisha ya wahitaji wengi hasa mama na mtoto kama tujuavyo kwenye wodi za kina mama na watoto  ambapo damu nyingi huhitajika"  alisema Mwanga.
Akizungumza kwa niaba  Mkuu wa Kitengo  Cha  Damu Salama Mkoa wa Ilala  Bernadetha Mshima alisema kuwa uchangiaji wa damu una faida  kwa jamii pia ni ibada kiimani kwani kila mtu anayetoa damu huwa hafahamu itakwenda kumsaidia nani.

Hafla hiyo ilikua ya kuwakaribisha wanafunzi wapya  wa mwaka wa kwanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...