Benki ya Equity (T)imetia saini Mkataba wa Makubaliano na Shirika la Posta nchini kutumiavituo vya Shirika hilo kutolea huduma za kibenki ili kusogezahuduma karibu na watanzania wengi zaidi.Akizungumza katika hafla ya utiaji saini mkataba huo jijini Dar esSalaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Equity Robert Kibotiamesema “Hatua hii itatuongezea wigo wamtandao wa utoaji huduma zetu ambazo ni nafuu zaidi nchini na hivyokuendana na lengo letu la kukomboa Watanzania kiuchumi kwakuongeza ushiriki wao katika mfumo rasmi wa fedha (financial inclusion).“Kwa sasa Equity Bank ina mawakala wapatao 3,900 na hivyo kuunganana Shirika la Posta kuwa kama Supa Wakala wetu , kupitia mtandao waofisi zake kutatuwezesha kuongeza idadi ya watuwatakaofikiwa na huduma zetu kwa ukaribu na urahisi zaidi. Kwakuanzia tutaanza na vituo 35 kwa maeneo ambayo hatukuwepo hapo awali" alisema.Kwa upande wake, Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la PostaTanzania, Macrice Mbodo amesema “Tunajivunia kuweza kuungana na Benki ya Equitykatika kufanikisha mpango huu utakaosaidia kufikisha huduma zakibenki kwa Watanzania wengi zaidi. Juu ya hilo kupitia mpango huuShirika la Posta pia litapata chanzo kipya cha mapato kupitia kamishenina hivyo kuimarisha mapato ya shirika”. Amesema.Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Equity Robert Kiboti akitia saini Mkataba wa Makubaliano na Shirika la Posta nchini.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Equity Robert Kiboti na Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la PostaTanzania, Macrice Mbodo Wakikabidhiana Mkataba huo.![]()
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...