Kwa mujibu wa wataalamu wa Afya, chanjo za COVID-19 zinafanya kazi kama chanjo nyingine. Chanjo husaidia mwili wa mtu kutambua na kupambana dhidi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa. Chanjo ya COVID-19 husaidia mwili kutambua na kupambana na virusi vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19. 

Je! Chanjo za COVID-19 zinatulinda jinsi gani? 

Chanjo za COVID-19 hufundisha mwili wako kutambua na kupambana na virusi vya COVID-19. Hazina COVID-19. Huwezi kupata ugonjwa wa COVID-19 kutoka kupata chanjo. Chanjo ni njia salama ya kujenga kinga dhidi ya virusi katika mwili, bila kusababisha ugonjwa. Chanjo za COVID-19 ambazo zilipitishwa kwa matumizi zimeonyeshwa kuwa nzuri sana katika kulinda dhidi ya ugonjwa mkali na kifo. 

Unaweza kuzungumza na daktari wako juu ya chanjo za COVID-19 na kwa nini chanjo ni sehemu muhimu ya kuitunza jamii kuwa salama na yenye afya. 

Je! Nitarajie madhara gani kutoka chanjo za COVID-19? 

Chanjo zote zinaweza kuwa na madhara kadhaa. Madhara haya kwa kawaida ni kidogo na hudumu kwa siku chache tu. Madhara ni pamoja na: • mkono wenye maumivu baada ya sindano • homa • kuumwa kwenye misuli • kuumwa kichwani. Hizi ni ishara kuwa chanjo inafaa. Kama una maswali yoyote au wasiwasi baada ya chanjo, wasiliana na kliniki yako ya chanjo au daktari yako.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...