· Washindi watatu wajinyakulia vifaa vya DJ zenye thamani ya milioni saba TSH kila mmoja.


Arusha. Bia pendwa ya Serengeti Lite imehitimisha shindano lake la DJs lililopewa jina la Take a Bite Out of Life kwa kuwatunuku ma-DJ watatu bora nchini vifaa vya kupigia mziki zenye thamani ya shilingi million saba kila mmoja kwenye ukumbi wa Triple-A ambapo ilishindanisha washiriki saba wa mwisho kutoka kanda tofauti nchini.

Tukio hili lilihitimisha kampeni ya miezi mitatu kwa kupata ma-DJ watatu kutoka kanda saba nchini. Pia washindi hawa wamepata fursa adimu za kuwa ma-DJ rasmi wa chapa ya Serengeti Lite katika promosheni na shughuli zake za utangazaji nchini.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha hafla hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Bia cha SBL, Nandy Mwiyombella, alisema, 'Ni wakati wa kusisimua kwa SBL na bia yake ya kipekee, Serengeti Lite, ambayo imetumia shindano hili ili kuwasaidia vijana kuonyesha vipaji vyao. Serengeti Lite ina shauku ya kuwaona vijana kuonyesha umahiri wao katika vipaji walivyonavyo’.

Aliendelea, ‘Vilevile shabaha ya Take a Bite out of Life ililenga kutoa burudani kwa wateja wetu katika maeneo waliyopo ili waendelee kufurahia kinwyaji chenye ladha kamili cha Serengeti Lite, Bia ya Kitanzania iliyotengenezwa kwa ajili ya Watanzania na ya Watanzania’.

Afisa Vijana wa Arusha Japhet Kurwa ndiye aliyeongoza hafla hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. John Mongella ambaye pia aliwatunuku washindi watatu waliobahatika. Kurwa alipongeza juhudi za SBL za kuchochea soko la ajira kwa kutoa motisha kwa vijana katika sekta ya burudani.

Kurwa alisema, ‘nimejawa na furaha kubwa sana baada ya kushuhudia jinsi vijana wanavyopambania ndoto zao kwa nguvu na ari. Nawapongeza sana SBL kwa kutimiza ndoto zao. Ni siku nzuri kwa washindi hawa watatu; maisha yao hayatakuwa sawa tena kwa sababu fursa hii imekuwa chanzo cha ajira kwao. Nina uhakika pia kuwa washiriki wengine (hasa washindi) mtaanza kupokea mialiko mingi kwenye hafla za kutumbuiza mziki maeneo mbalimbali na pengine kufungua studio zenu za muziki hapo baadae.

Kurwa aliendelea kusema, ‘tukio la leo limekuwa gumzo na kuibua hisia nzuri sana kwa vijana hapa mjini Arusha. Ni matumaini yetu kama Serikali ya mkoa kuwa vijana wamehamasika kujiinua kimaisha na kuchangamkia kila fursa zingine zilizopo ili kufikia malengo yao hasa katika hiki kipindi ambacho Serikali yetu inafanya kazi kubwa ya kuongeza ajira nchini’.

Kampeni ya Take a Bite Out of Life iliambatana na shughuli za burudani kutoka ma-DJs wa ndani walioshindana katika wilaya na mikoa nchini kote. Shindano hili lilishirikisha zaidi ya washindani 5,200 wenye zaidi ya miaka 18 wenye matarajio ya kujenga vipaji vyao kama waburudishaji wa muziki.

Katika kila tukio, washiriki waliobahatika waliondoka na zawadi mbalimbali na zaidi ya hayo jukwaa hili liliwapa fursa ya kuonyesha vipaji vyao mbele ya majaji maarufu kama vile DJ ZERO na umma kwa ujumla.

Hii si mara ya kwanza kwa SBL kuwekeza katika miradi kama hii. SBL pia imewekeza katika sekta ya michezo kwa kudhamini timu ya Taifa Stars, ligi ya Taifa ya Wanawake na mashindano mengine muhimu ya gofu.

Mkuu wa Kitengo cha Bia wa Kampuni ya  Serengeti (SBL), Nandy Mwiyombella (kulia) na Katibu wa chama cha MaDJ nchini, Asanterabi Mtaki (kushoto) wakimkabidhi tuzo ya mshindi wa kwanza wa shindano la DJ compee, Take a Bite Out of Life, Abdulaziz Juma maarufu Dj Dully Tz kutoka Dodoma,  ambaye pia alipata seti ya vyombo vya muziki wa uDJ vyenye thamani ya shilingi milioni 7 kutoka kampuni ya SBL. Shindano hilo lililowashirikisha  wachezesha muziki  zaidi ya 5,200 kote nchini na fainali zake zilifanyika  jijini Arusha usiku kuamkia jumapili.

Mkuu wa Kitengo cha Bia wa Kampuni ya  Serengeti (SBL), Nandy Mwiyombella akimkabidhi zawadi mshindi wa tatu wa shindano la DJ compee, Take a Bite Out of Life, Mussa Shaban maarufu Dj. Son kutoka mkoa wa Kilimanjaro shindano hilo lililoandaliwa na kampuni ya bia ya Serengeti Tanzania SBL lenye lengo la kuwasaidia vijana kuweza kujiajiri.



Meza ya majaji ikiongozwa na Jaji mkuu, John Dilinga (katikati), Katibu chama cha maDj Tanzania, Asanterabi Mtaki (kushoto) na Fadhili Jeremiah maarufu Dj Dhifa

Afisa anayeshughulika na masuala ya vijana wa Mkoa wa Arusha, Japhet Kurwa (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Basata, Matiko Mniko (kushoto) na Afisa Sanaa wa Basata, Joseph Mmbigo.

Washiriki waliongia mchujo wa 5 bora wakiwa kwenye picha ya pamoja kabla ya kumpata mshindi wa shindano la DJ compee, Take a Bite Out of Life jijini Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...