Na Pamela Mollel,Arusha

Viongozi wa dini wametakiwa kuunga mkono jitihada za serikali katika kuhamasisha jamii kuhusu chanjo dhidi ya maambuziki ya ugonjwa hatari wa korona ikiwa ni sehemu ya kupambana na janga hilo.

Hayo yameelezwa na imamu wa msikiti wa Zahara, Maulidi  Sombi katika maadhimisho ya Maulidi yaliyofanyika hivi karibuni katika eneo la Makumbusho jijini Arusha ikiwa ni kumbukumbu ya kuzaliwa Kwa mtume Mohammad ambapo alidai lengo la Maulidi hayo Kwa mwaka huu ni kufufua mioyo ya Watu ili kurejesha mshikamano na upendo.

Sombi alisema kuwa jamii inapaswa kushiriki vyema katika zoezi la sensa hapo mwakani kuomba waumini kote nchini walio na dini na wasio na dini kushirikiana na serikali katika kufanikisha zoezi hilo ambalo litasaidia kuleta maendeleo kwa watanzania kujulikana idadi kamili

Naye Naibu Katibu mkuu jumuiya ya Maridhiano Tanzania,Abdulazack Amiri alisema lengo la maadhimisho hayo ni kuhimiza maadili mema Kwa waumini na Jamii Kwa ujumla kuepua kujiingiza katika matendo maovu yesiompendeza mwenywzi mungu.

Kwa upande wake sheikh Mlewa shabani Kimwaga kutoka Mkoani Kilimanjaro alisema kuwa maadhimisho ya Maulidi yanalenga  kuikumbusha Jamii kuhusu malezi Bora Kwa Jamii na watoto ikiwa ni njia sahihi ya kumwenzi mtume Mohammad

Nao waumini walio udhuria maadhimisho hayo walisema wamefuraishwa na mafundisho yaliotolewa na viongozi hao wa dini kwani kwa sasa ni kweli jamii imekosa maadili na kusau dini 

Waliongeza kuwa watahakikisha wanaunga mkono serikali juu ya mapambano dhidi ya ugonjwa hatari wa corona

Imamu wa msikiti wa Zahara,Maulidi Sombi akizungumza katika maadhimisho ya Maulid yaliyofanyika jijini Arusha hivi karibuni
Viongozi wa dini wakifuatilia maadhimisho ya Maulid yaliyofanyika jijini Arusha hivi karibuni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...