Mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, Waziri wa Nchi Afisi ya  Rais , Fedha na Mipango, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Jamal K. Ali,  alipotembelea katika banda la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).  Maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha kitaifa yanaendelea katika viwanja  vya Mnazi Mmoja ambapo NSSF inaendelea kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa sekta binafsi na sekta isiyo rasmi.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba akipata maelezo kutoka kwa Afisa matekelezo mwandamizi Hawa Godigodi, alipotembelea banda la NSSF wakati wa Maonesho  ya Wiki ya Huduma za Fedha kitaifa katika viwanja  vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii(NSSF) Masha Mshomba akielezea huduma mbalimbali zinazotelewa na NSSF katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa. Katika maadhimisho hayo NSSF inatoa elimu kuhusu hifadhi ya jamii, elimu kuhusu umuhimu wakujiwekea akiba, elimu ya  huduma zinazotolewa kwa njia  ya  mtandao ambapo ndio kipaumbele muhimu cha Mfuko pamoja na kueleza fursa za uwekezaji.
Mkurugenzi wa Idara ya Hifadhi ya Jamii, Ofisi ya Waziri Mkuu, Festo Fute (katikati) akisisitiza jambo alipotembelea banda la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wakati wa Maonesho ya Wiki ya Huduma za iFedha kitaifa katika viwanja  vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba, kulia ni Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma, Lulu Mengele  pamoja na wafanyakazi wa  NSSF
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. John Mduma (kulia), akipata maelezo mbalimbali kuhusu ushiriki wa NSSF katika  Maonesho ya Wiki ya Huduma za  Fedha kitaifa. Maonesho haya yanaendelea katika viwanja vya Mnazi mmoja, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa  Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi Afisi ya  Rais , Fedha na Mipango, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Jamal K. Ali kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na NSSF wakati wa  Maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha kitaifa katika viwanja vya Mnazi mmoja.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko  Taifa wa Hifadhi ya Jamii  (NSSF), Masha Mshomba (wa kwanza mstari wa mbele)  akiwa katika ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam
Waziri wa Nchi, Afisi ya  Rais Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Jamal K. Ali (aliyekaa katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Kamishna Uendelezaji wa Sekta ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha Dkt. Charles Mwamwaja (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Fatma Nyangasa na viongozi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa  wa Hifadhi  ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba, akiwa katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa ambapo alipata fursa ya  kutembelea na kupata maelezo katika banda la Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi  (WCF) na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF). Mifuko hiyo ipo katika viwanja vya Mnazi mmoja kutoa elimu kuhusu  huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wanachama wao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...