Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV


SERIKALI kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imeandaa maadhimisho ya wiki ya huduma ya fedha kitaifa ambayo yatafanyika Novemba 8 hadi Novemba 11 mwaka huu lengo likiwa kujenga uelewa na weledi kwa umma katika matumizi sahihi ya huduma za fedha zinatolewa.

Akizungumza wakati akifungua semina ya siku moja kwa wahariri wa vyombo mbali mbali vya habari nchini kuhusu masuala ya fedha na maadhimisho ya wiki ya huduma za fedha kitaifa ,Katibu Mkuu Wizara ya fedha na Mipango ndugu Emmanuel Tutuba amesema katika wiki hiyo Wizara imejielekeza katika masuala mbalimbali yakiwemo kuimarisha ufanisi wa masoko ya fedha kupitia elimu ya fedha,kuongeza upatikanaji wa huduma za fedha.

‘’Hatutaishia hapo tutatoa elimu ya kuwezesha kumlinda na mtumiaji wa huduma za fedha,kuwezesha wananchi kusimamia vizuri rasilimali fedha,kuwawezesha wajasiriamali wadogo kuongeza ujuzi na matumizi sahihi ya huduma za fedha katika kukuza biashara zao,kuimarisha utamaduni na kujiwekea akiba,kukopa na kulipa madeni na kuongeza mchango wa sekta ya fedha kwa ukuaji wa uchumi,’amesema.

Aidha ametoa mwito kwa vijana kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo katika kujifunza kwa kuwa sekta hiyo imejipanga kuwahudumia vizuri ili kuwawezesha kutizama na kuchangamkia fursa katika wizara hiyo.

Ameongeza Wizara hiyo imejipanga vizuri kuhakikisha inatatua changamoto ikiwemo ya uelewa mdogo wa masuala ya fedha,uelewa mdogo wa bidhaa zitolewazo na watumiaji na watoa huduma za fedha,matumizi ya huduma za fedha zisizo rasmi,ambapo utekelezaji wa programu hiyo inakusudiwa ifikapo 2025,takribani asilimia 80 ya wananchi wawe wamepata uelewa wa masuala ya fedha.

Maadhimisho hayo kitaifa yatafanyika jijini Dar es Salaam na kubebwa na kauli mbiu isemayo ‘’Boresha Maisha kupitia Elimu ya Fedha’’.


Katibu Mkuu na Mlipaji Mkuu wa Serikali Wizara ya Fedha na Mipango Emmanuel Tutuba akizungumza leo Novemba 1,2021 jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa Semina ya Wahariri wa Vyombo vya Habari na Waandishi wa habari kwa ajili ya kuwajengea uwezo kuhusu masuala ya Fedha na maadhimisho ya wiki ya Huduma za Kifedha Kitaifa inayotarajiwa kuanza Novemba 8-14 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Kauli mbiu kwenye maadhimisho hiyo imetajwa kuwa ni ‘Boresha Maisha kupitia Elimu ya Fedha’.

Kamishna Idara ya Maendeleo ya Sekta ya Fedha Wizara ya Fedha Dkt. Charles Mwamwaja akitoa maelezo ya kikao kazi hicho kabla ya kufunguliwa kati ya Wizara ya Fedha na Wahariri wa Vyombo vya habari mbalimbali nchini, Kikao hicho pamoja na mambo Kadhaa kinajadili kuhusu Sekta ya Fedha na Maadhimisho ya wiki ya Huduma za Kifedha Kitaifa ambacho kinafanyika kwenye ukumbi wa Kambarage Ofisi ya Hazina jijini Dodoma.
Kaimu Kamishna Msaidizi Idara ya Uendelezaji Sekta ya Fedha, Bi. Dionisia Mjema akisikiliza maswali kutoka kwa washiriki wa mkutano huo mara baada ya kuwasilisha mada yake kuhusu Wasilisho la Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha.

Kaimu Kamishna Msaidizi Idara ya Uendelezaji Sekta ya Fedha, Bi. Jannet Hiza akitoa mada kuhusu Programu ya Kutoa Elimu kwa Umma ya Mwaka 2021/22-2025/26.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu Serikali Bw. Emmanuel Tutuba kulia ,Kamishna Idara ya Maendeleo ya Sekta ya Fedha Dkt. Charles Mwamwaja pamoja na Kamishna Msaidizi Wizara ya Fedha Dionisia Mjema 


Afisa Uhusiano, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Zanzibar, Bi. Asha Hussein Saleh (kushoto) na Bw.Salim Kimaro, Afisa Msimamizi Mkuu wa Fedha, Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha

Baadhi ya maafisa habari kutoka taasisi zilizo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kweye mkutano huo.



Baadhi ya Wahariri wa Habari wakifuatilia mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye mkutano huo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Fedha Bw. Benny Mwaipaja akitoa ratiba na miongozo mbalimbali katika mkutano huo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...