Naibu Katibu Mkuu ametoa maelekezo hayo leo jumatano 26 Januari, 2022 katika ziara ya wajumbe wa Sekretarieti ya HKT inayoendelea Visiwani Zanzibar, alipokuwa akikagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya wilaya ya Kaskazini A inayogharimu shilingi Bilioni 4.4 iliyoanza kujengwa mwezi Januari mwaka huu na ikitarajiwa kukamilika mwezi Juni, mwaka huu.
Naibu Katibu Mkuu akitoa maelekezo hayo baada ya kukagua na kuridhishwa na ujenzi unaoendelea, ambapo amesema kuwa utamaduni wa WanaCCM ni kusaidia katika maendeleo na ujenzi wa nchi yetu, hivyo akitoa maelekezo hayo amesema,
"Naagiza Umoja wa Vijana wa CCM Zanzibar, tuwalete hapa vijana watekeleze Ilani ya Uchaguzi na kujenga Taifa, na kwa upande wa chama naagiza Makatibu wa Mikoa yote ya Unguja na Pemba kupanga ratiba ya matawi ya CCM katika maeneo husika yawe yanashiriki katika ujenzi wa Hospitali katika wilaya zote za Zanzibar, na hiyo ndio asili tuliokuwa nayo Chama Cha Afro Shiraz Party na TANU na sasa ni CCM"
Nitapita kukagua namna makatibu wa mikoa mlivyoyapanga matawi katika kutekeleza hilo na vijana wa umoja wa vijana wa CCM mnavyotekeleza maagizo haya, Naibu Katibu Mkuu amesisitiza.
Mkuu wa mkoa wa Kaskazini Unguja Ndg. Ayoub Mohammed Mahmoud akitoa maelezo ya ujenzi wa hospitali Katika Mkoa wa Kaskazini Unguja, amesema kuwa,
"Katika Mkoa Hospitali ya Kivunge inajengwa ambayo ujenzi unaendelea na unagharimu shilingi bilioni 4.8, na hapa Kaskazini A hospitali inajengwa kwa shilingi bilioni 4.4 na ni eneo ambalo linauhutaji mkubwa wa hospitali ya wilaya."
Miradi hii itachukua miezi sita kukamilika ambapo imeanza mwezi Januari mpaka Juni 2022, Mkuu wa Mkoa ameongeza.
Katika hatua nyingine Naibu Katibu ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa kilimo cha umwagiliaji mpunga Kibokwa, mradi wa upanuzi wa gati bandari ya mkokotoni, mradi wa eneo maaluma la viwanda Pangatupu, mradi wa maboresho ya bandari ya bumbwini/Pangapwani, pamoja na kuzungumza na wanachama katika mikutano ya mashina.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (Zanzibar) Dkt. Abdalla Juma Sadala akishiriki ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Kaskazini B, mkoa wa Kaskazini Unguja ikiwa sehemu ya ziara ya Ukuaguzi, Usimamiaji, Uhamasishaji na Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020 – 2025 pamoja na kukagua uhai wa CCM katika ngazi za mashina. (Picha na CCM Makao Makuu)
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (Zanzibar) Dkt. Abdalla Juma Sadala akipata maelezo ya kitaalamu kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Zanzibar Ndugu Nahat Mohammed Mahfoudh (kulia) juu ya ujenzi wa juu ya ujenzi wa bandari Mkokotoni, Kaskazini A, mkoa wa Kaskazini Unguja katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe.Ayoub Mohammed Mahmoud ikiwa sehemu ya ziara ya Ukaguzi, Usimamiaji, Uhamasishaji na Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020 – 2025 pamoja na kukagua uhai wa CCM katika ngazi za mashina. (Picha na CCM Makao Makuu).Picha zaidi za Ziara ya Naibu Katibu Mkuu CCM ( Zanzibar)Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (Zanzibar) Dkt. Abdalla Juma Sadala akizungumza na wanachama wa Tawi la CCM Mahonda B, mkoa wa Kaskazini Unguja ikiwa sehemu ya ziara ya Ukaguzi, Usimamiaji, Uhamasishaji na Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020 – 2025 pamoja na kukagua uhai wa CCM katika ngazi za mashina. (Picha na CCM Makao Makuu)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...