Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam 

KAMPUNI ya JK White Cement, Tanzania imeendelea kutambua mchango wa Wadau wake waliopo sehemu mbalimbali nchini kwa kuwakabidhi zawadi mbalimbali baada ya kufanya vizuri katika matumizi ya bidhaa zao kupitia promosheni maalum ya Faidika na Bidhaa mpya ya JK Wall Putty iliyotambulishwa mwaka 2021.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, jijini Dar es Salaam, Meneja Mauzo na Masoko wa Kampuni hiyo, Felista Masabo amesema wametoa zawadi hizo ili kuthamini na kutambua mchango wa Wadau wake ambao ni Wauzaji, Wanunuaji na Watumiaji waliopo sehemu mbalimbali nchini.

Masabo amesema lengo kubwa la kutoa zawadi hizo ni kuwapa mkono wa ahsante sambamba na kuwashukuru kwa mchango wao Wadau hao katika matumizi ya bidhaa zao sanjari na kugawana kinachopatikana kupitia bidhaa hizo.

“Watumiaji ambao ni Mafundi Rangi, tumewazawadia zawadi kwa kutambua mchango wao kwetu, wametuunga mkono, na kututhamini, tunaamini wao ni Wadau wetu tunataka, sisi tupate na wao wapate, pia tunataka kila anayetumia bidhaa zetu awe mshindi”, amesema Masabo.

Kwa upande wao Washindi wa Promosheni hiyo wamesema bidhaa za JK White Cement ni nzuri kwa matumizi ya ujenzi, zimewasaidia kwa kiasi kikubwa katika shughuli zao za ujenzi.

“Natumia sana bidhaa zao (JK White Cement) zinatoa Fangasi za ukutani kwa kiasi kikubwa, mara kwa mara huwa natumia na inapendezesha ukuta”, amesema Yassin Yassin.

Washindi hao watatu wamepatikana kupitia Promosheni hiyo ya JK Wall Putty iliyoanzishwa mwaka jana, Washindi hao ni Yassin Yassin kutoka mkoa wa Mwanza, ambaye amezawadiwa Jokofu, mshindi wa pili ni Weston Komba kutoka Dar es Salaam amezawadiwa Runinga na vifaa mbalimbali vya ujenzi na mshindi wa tatu Michael Ernest kutoka mkoa wa Dodoma ambaye amezawadiwa Radio kubwa (Subwoofer).
Meneja Mauzo na Masoko wa Kampuni ya JK White Cement, Tanzania , Felista Masabo akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wakitangaza Washidi watatu kutoka mikoa mbalimbali nchini wa Promosheni ya ya Faidika na Bidhaa mpya ya JK Wall Putty, hafla hiyo ya ugawaji wa zawadi hizo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa JK White Cement, Manish Shrivastava akikabidhi zawadi kwa Mshindi wa kwanza wa Promosheni ya Faidika na Bidhaa mpya ya JK Wall Putty iliyoanzishwa mwaka 2021 kwa lengo la kutambua, kuthamini mchango wa Mafunzi Rangi kupitia bidhaa za Kampuni hiyo kwa wadau wake, wa kwanza kulia ni Meneja Mauzo na Masoko wa Kampuni ya JK White Cement, Tanzania, Felista Masabo akishuhudia.
Picha ya pamoja kati ya Wafanyakazi wa Kampuni ya JK White Cement, Tanzania na baadhi ya Wauzaji, wanunuaji na watumiaji wa bidhaa za Kampuni hiyo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...