WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watanzania kushirikiana na kushikamana ili kuyapa thamani madini ya Tanzanite na kuifanya dunia nzima itambue kuwa madini ya Tanzanite yanapatikana Tanzania tu na tayari imeweka mazingira ya kuyaongezea thamani.

 

Mheshimiwa Majaliwa ameyasema hayo leo (Jumatano, Januari 26, 2022) alipozungumza na wananchi katika eneo la EPZA unapojengwa Mji wa Tanzanie katika Mji Mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani Manyara.

 

Waziri Mkuu amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan itahakikisha rasilimali zote zilizoko nchini yakiwemo madini ya Tanzanite zinawanufaisha wananchi wote hususani wanaoishi katika maeneo zinapopatikana. “Watanzania lazima tushirikiane na tushikamane kuyapa thamani madini hayo.”

 

Amesema kuwa Serikali itaendelea kukutana na wafanyabiashara wa sekta madini kwa lengo la kuhakikisha kwa pamoja wanaweka mikakati ya kusaidia kuikuza sekta hiyo ili iendelee kuleta tija kwa watanzania na taifa kwa ujumla.

 

Akizungumza baada ya kukagua eneo la uwekezaji la EPZA, Waziri Mkuu amewataka watanzania kujitokeza na kuwekeza katika eneo hilo “Watanzania tumieni fursa ya eneo hili kuwekeza mtakapa faida”

 

Mheshimiwa Majaliwa aliwasisitiza wananchi waendelee kufanya biashara hiyo ambayo ina manufaa makubwa kwao na Taifa kwa ujumla na kwamba Serikali ipo tayari kuwahudumia wakati wote. “Tumejipanga kuwahudumia iwe wakati wa jua au wakati wa mvua.”

 

Naye, Naibu Waziri Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amemuahidi Waziri Mkuu kuwa watahakikisha wanasimamia ujenzi wa eneo hilo ili liweze kukamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma iliyokusudiwa kwa watanzania wenye nia ya kuwekeza.

 

Awali, Mheshimiwa Majaliwa alitembelea na alikagua soko la madini ya Tanzanite la Tanzanite Forever Lapidary ambapo alishuhudia hatua mbalimbali za uchenjuaji wa madini hayo pamoja na namna biashara hiyo inavyofanyika kwa njia ya uwazi.

 

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanzanite Forever Lapidary, Faisal Juma Shahbhai alisema licha ya maboresho yaliyofanyika katika sekta ya madini, pia ameishauri Serikali iweke mipango mahsusi itakayolinufaisha zaidi Taifa kiuchumi kutokana na uwepo wa madini hayo.

 

“Sasa biashara inafanyika kwa urahisi, sisi wafanyabiashara wa madini ya Tanzanite tunaridhishwa na utendaji kazi wa Serikali kwani tupo katika mfumo mzuri sana. Naishauri Serikali ihakikishe wafanyabiashara wanakua specific ili tuyatendee haki madini haya.”

 

Pia ameishukuru serikali kwa uamuzi wa kuelekeza biashara ya madini ya tanzanite ifanyike katika eneo la mirerani yanakopatikana madini hayo kwa sababu imewezesha wakazi wa maeneo hayo kunufaika.

 

Naye, Kaimu Afisa Madini Mkazi, Mirerani Fabian Mshai amesema tangu kuboreshwa kwa kanuni ili kuruhusu buiashara na uongezaji thamani madini ya Tanzanite kufanyika Mirerani hadi sasa jumla ya wafanyabiashara wakubwa wa madini 48 wananunua madini hayo na kuyachakata kutoka kwa wachimbaji na wafanyabiashara wadogo wa madini hayo.

 

“Tangu kuanzishwa kwa biashara na uongezaji wa thamani wa madini ya Tanzanite Mirerani, mpaka sasa jumla ya Vibali 105 vya usafirishaji wa madini hayo nje ya nchi vimetolewa kwenda nchini India, Ujerumani, China, Marekani, Thailand, Uingerea, Uhispania na Uswisi”

 




 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akionyeshwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanzanite Forever Lapidary, Faisal Juma Shabhai, madini ya Tanzanite ambayo yamechongwa na kampuni hiyo iliyopo kwenye jengo la Soko la madini, Mererani wilayani Simanjoro, Januari 26, 2022. Alikuwa katika ziara ya kikazi ya mkoa Manyara. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishudia uchongaji wa madini ya Tanzanite uliokuwa ukifanywa na mtalaam, Jackline Saibulu wakati alipotembelea Kampuni ya Tanzanite Forever Lapidary iliyopo kwenye jengo la Soko la Madini, Mererani wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara, Januari 26, 2022. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama kazi ya kuchonga madini ya Tanzanite wakati alipotembelea Kampuni ya Tanzanite Forever Lapidary iliyopo kwenye jengo la Soko la Madini, Mererani wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara, Januari 26, 2022. Watalaamu hao wa kuchonga madini ni Jackline Saibulu (kushoto) na Dorcas Steven. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama Tanzanite iliyochongwa wakati alipotembelea Kampuni ya Tanzanite Forever Lapidary iliyopo kwenye jengo la Soko la Madini, Mererani wilayani Simanjiro Januari 26, 2022. Kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Faisal Juma Shahbhai. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa amevaa miwani maalum wakati alipokagua ubora wa madini ya Tanzanite katika kampuni ya Tanzanite Forever Lapidary iliyopo kwenye jengo la Soko la Madini, Mererani wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara, Januari 26, 2022. Alikuwa katika ziara ya kikazi ya mkoa huo. Kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Faisal Juma Shahbhai. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...