Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amewakaribisha wafanyabiashara kutoka Ufaransa kuwekeza Tanzania katika sekta za mifugo, kilimo, nishati, madini na maeneo mengine yenye fursa.

Rais Samia ametoa rai hiyo wakati akilihutubia Shirikisho la Biashara la Ufaransa (MEDEF) mjini Paris, Ufaransa na kuongeza kuwa serikali yake inachukua hatua muhimu kuweka mazingira muafaka ya kukuza sekta binafsi.

Rais ameeleza kuwa Serikali imefanya mabadiliko makubwa ya kisheria na kitaasisi kwenye sekta binafsi kuhakikisha kuna wepesi wa kuanzisha na kufanya biashara nchini.

Rais Samia amesisitiza kuwa jitihada za serikali yake zimeendelea kuleta matokeo chanya, kama vile kituo cha uwekezaji kimesajili miradi 256 mwaka 2021 inayotarajiwa kuzalisha ajira 53,025 na mtaji wa dola za kimarekani bilioni 3.749.

Wakati huo huo, nchi hizo mbili zimetia saini Hati ya Makubaliano kati ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania na kampuni ya Kimataifa ya Bouygues Bâtiment kwa ajili ya ukarabati wa jengo la pili (Terminal II) la abiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.

Upande wa Tanzania katika hatua ya utiaji saini

ulifanywa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi - Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Ally Possi huku Ufaransa ukiwa umewakilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya kimataifa ya Bouygues Batiment (BBI), Bw. Eric Fleurisson.

Ufaransa unashika nafasi ya 35 kwa uwekezaji nchini Tanzania, ambapo tayari kuna miradi 40 yenye thamani ya dola milioni 73.4 za Marekani, na kuzalisha ajira 1,885 kufikia sasa.


Zuhura Yunus

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.
 
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...