Wanawake wamedokezwa juu ya umuhimu wa kukuza vipaji vyao vya uongozi katika zama hizi za kampuni kubwa na kufanya kazi kwa pamoja kwa mashirika.

Hayo yalisemwa kwenye tukio maalumu lililoandaliwa na kampuni ya SGA Security, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Wapendanao, ambapo wafanyakazi wanawake ambao ni 6,000 nchini walipokea ukufunzi maalumu juu ya uongozi na namna ya kukabili hisia kwa njia chanya.

Tukio hilo liliwezeshwa Mzungumzaji Mtoa Motisha maarufu, George Obado, ambaye ni mtaalamu kwenye masuala ya uongozi, na Ruth Serem, mtaalamu katika masuala ya uwezeshaji wanawake, akiwapitisha wanawake katika hatua mbalimbali na sifa za kile wataalamu wanachoita ‘mwanamke asiye wa kawaida’. Kundi la wawakilishi kutoka sehemu mbalimbali za SGA ilidokeza juu ya namna ya kukabili hisia, ikiwa ni somo la wkaati huu kwa viongozi kwenye dunia ya leo ya kampuni kubwa kubwa.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa SGA Tanzania, Eric Sambu, alirejea kwamba wanawake wanahusika kwa kiasi kikubwa katika utoaji wa uamuzi wa kimkakati. Alieleza jinsi wanawake walivyo na zawadi ya kiasili katika kusimamia na kutatua hali mbaya na mara nyingi hufikiria sababu zote zinazoweza kuathiri lengi na hivyo wakati mwingi huwa sawa katika waamuayo na kufanya.

Aliwahimiza wanawake kujiamini na kutumia faida za zawadi zao za asili kujipandisha wnyewe kwenye nafasi za ushawishi kwenye ulimwengu huu wa ushirikiano. Aliwasahauri dhidi ya kuwaona wenzao kuwa kana kwamba wapinzani, badala yake wajielekeze kwenye  kutwaa kinachopatikana kwenye kujuana kwao na kufanya kazi pamoja.

Bw George Obado alirejea juu ya haja kwa wanawake kujitambua, kudhibiti na kuhamasishana wenyewe na kumudu vyema uhusiano, wakitazama pia wajibu wao kijamii. Aliwashauri wawe na tunu binafsi na kumudu vyema na kiutu uzima mihemko na ili kuganya hayo, wanatakiwa kuelewa juu ya nguvu na udhaifu wao.

Ruth Serem naye alitoa vidokezo juu ya jinsi ya kuwa mwanamke wa kitofauti au asiye wa kawaida, akachukua kile alichiopata kusema Maya Abgtelou, kwamba wamefanywa kuwa maalumu, na kwa hakika si watu wa kawaida.
Meneja Rasilimaliwatu wa SGA Security, Bw Ebenezer Kaale, alisema kwamba kampuni hiyo inawapa moyo wanaume katika nafasi zao kuendelea na ustawi, akisema ndiyo siri ya mafanikio yao.

“Japokuwa sekta ya usalama haijavuta wanawake wengi, SGA imejenga mazingira sawa na inao wanawake wengi kwenye safu muhimu na uzoefu unaonesha kwamba kwamba wamekuwa si wa kawaida,” alisema. “Wanawake ni waangalifu zaidi huku wakifuata sera na kanuni zilizowekwa na kwa mara nyingi ni waaminifu, na hizi ndizo sifa muhimu kwenye sekta hii,” akaongeza.

SGA Security ni moja ya waajiri wakubwa zaidi nchini na kampuni kongwe zaidi ya ulinzi, ikiwa imefanya shughuli zake tangu 1984. Hutoa huduma maalumu katika ulinzi na usimamizi wa fedha taslimu, suluhishio kwenye ulinzi wa kielektroniki, huduma za mwitikio wa dharura pamoja na huduma za usafirishaji.
Baadhi ya waajiriwa wanawake wa kamouni ya SGA Security wakisherehekea Siku ya Wapendanao Jumatatu iliyopita. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa SGA Tanzania, Eric Sambu na Mzungumzaji Mtoa Motisha, George Obado



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...