Kwa masikitiko makubwa familia ya Kubaga ya Chang’ombe Dar es salaam inawataarifu habari za kufariki kwa Mzee wetu Lay Canon Raphael Kubaga, baba mzazi wa Tino Kubaga ambaye ni Mshauri wa Walei, Mwenyekiti wa Ubaki, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Halmashauri ya Mtaa wa Mt. Albano. 


 Umauti umemfika Mzee Kubaga leo majira ya saa sita adhuhuri katika hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es salaam ambako alikuwa amelazwa kwa matibabu. 


Mipango ya mazishi inaendelea nyumbani kwake Chang’ombe TCC Club na matarajio kwa sasa ni kuwa mwili wa marehemu utapumzishwa siku ya Jumatatu. 

 

Tutaendelea kuwaletea taarifa kadri tutakavyozipokea. Kwa sasa tuungane katika sala kuiombea faraja familia, ndugu na jamaa. Roho yake Mzee Kubaga ipate pumziko la amani milele.

- Amina.


 Pichani mbele kushoto ni marehemu Mzee Paphael Kubaga enzi za uhai wake akiwa na Augustino "Tino" Kubaga (Mtoto wake wa Kwanza nyuma ya Baba yake) Oliver Kubaga na mama Kubaga. Upande wa kulia ni  Raphael Kubaga(Kivugu) na  katikati ni mabinti zake wawili, Betty Kubaga na Suzana Kubaga.


Marehemu Mzee Kubaga alikuwa Afisa Uhamiaji  Mkuu mstaafu (1969-1983) na pia Mwenyekiti wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) kwa muda mrefu. 

Katika wakati wake alipokuwa Mkurugenzi wa Uhamiaji Mzee Kubaga anakumbukwa kwa  mchango mkubwa katika fani ya michezo ambapo  alisisitiza na kusimamia kwa umahiri michezo Idarani humo kama vile Mpira wa miguu, Mchezo wa Ngumi, Mchezo wa mpira wa Pete, Mpira wa kikapu, bila kuwasahau wanariadha  mahiri kiasi hata  idara ilijizolea sifa nyingi kutokana na michezo kiasi ya kwamba wanariadha na mabondia wengi wazuri walikuwa wakitokea katika idara ya Uhamiaji,nao waliweza kuwakilisha nchi nje ya nchi na kufanya vizuri.


Vijana wengi walifaidika kupitia michezo na kwa sasa wamekuwa wakitoa mchango mkubwa katika nchi hii katika maswala ya ulinzi na usalama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...