NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MOROGORO.

KATIBU Mkuu wa TUGHE taifa Bw. Hery Mkunda amepongeza Uhusiano mzuri baina ya Menejimenti ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Wafanyakazi .

Bw. Mkunda ameyasema hayo mjini Morogoro Februari 11, 2022 wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi la WCF.

“Baraza la Wafanyakazi ni chombo cha ushauri kwa Menejimenti na kinawakilisha wafanyakazi kutoka idara na mikoa , nimeona kuna ushirikishwaji mkubwa kwenye taasisi hii ukilinganisha na taasisi nyingine, naomba niwapongeze sana.” Alisema Bw. Mkunda

Aliwakumbusha wafanyakazi wajibu wao kwa mwajiri  “Kudai maslahi ni jambo moja lakini pia lazima wafanyakazi watambue kuwa wanao wajibu wa kwenda kufanya kwa mwajiri ili kuhakikisha yale maslahi ambayo wafanyakazi wanadai yawe na uhalali.” Alifafanua.

Awali  Mwenyekiti wa TUGHE tawi la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bi. Amina Likungwala aliupongeza  Uongozi wa Mfuko kwa mahusiano mazuri na Wafanyakazi.

"Napenda kuipongeza Menejimenti ya WCF kwa mahusiano mazuri na Wafanyakazi, na ushirikiano ndani ya Baraza hili, kwakweli tunapata ushirikiano wa kutosha na tunajadiliana kwa uwazi" Alisema.

Alisema hoja za wafanyakazi zilizopelekwa kwenye Menejimenti kwa kiasi kikubwa zimefanyiwa kazi na TUGHE ina imani hata zile hoja zilizosalia nazo zitafanyiwa kazi.

Aidha, Katibu wa TUGHE mkoa wa Dar es Salaam, Bi. Sara Rwezaura aliwahimiza wafanyakazi ambao hawajajiunga na TUGHE wafanye hivyo kwani ni chombo muhimu kwa wafanyakazi.

Akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa Baraza ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma  alisema maamuzi yanayopitishwa ndani ya Baraza ni kwa ajili ya  maslahi ya Taasisi na ndio maana baraza hili lina umuhimu mkubwa.

“Sisi tumekuja hapa kwa uwakilishi, tuendelee kuwahamasisha wenzetu kwa kuwapa mrejesho kutokana na maamuzi tuliyofikia.” Alisema.

Baadhi ya wajumbe wakimsikiliza mtoa mada kutoka Ofisi ya Kazi, Mkoa wa Morogoro
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi (WCF) ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo, Dkt. John Mduma
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wafanyakazi (TUGHE) Taifa, Bw. Hery Mkunda.

Mwenyekiti wa TUGHE tawi la WCF, Bi. Amina Likungwala.
Katibu wa TUGHE mkoa wa Dar es Salaam, Bi. Sara Rwezaura.
Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu WCF, Bw. Julius Lwenje.
Bi. Felister Buzuka, mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi WCF, akiagana na wajumbe wenzake ambapo anatarajia kustaafu utumishi wa umma mwezi ujao.

Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi WCF, Dkt. John Mduma na Katibu wa Baraza, Bi. Irine Mungure.
Katibu Msaidizi wa Baraza, Bw. Thadei Kimati.
Katibu (mstaafu) wa Baraza la Wafanyakazi WCF, ambaye kwa sasa ni Meneja Rasilimali Watu Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Bw. Mbarikiwa Masinga.
Mwenyekiti wa Baraza, Dkt. John Mduma (kushoto), akimkabidhi Katibu (mstaafu) wa Baraza la Wafanyakazi WCF, Bw. Mbarikiwa Masinga Mfuko wenye machapisho ya taarifa za Mfuko.

Katibu (mstaafu) Bw. Mbarikiwa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa baraza.

Mkurugenzi wa Fedha, Mipango na Uwekezaji, WCF, Bw. Bezil Ewala.
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar.
Mkurugenzi wa Uendeshaji, WCF, Bw. Anselim Peter

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...