Waandaaji wa mbio maarufu za Kilimanjaro Premium Lager Marathon 2020 wamesema kuwa licha ya usajili wa mbio za Km 42 na Km 21 kufungwa baada ya kujaa, usajli wa mbio za Km 5 bado unaendelea kwa njia ya Tigo Pesa.  

Taarifa iliyotolewa Jijini Dar es Salaam ilisema kuwa usajili wa mbio za Km 42 na 21 ulifungwa tangu Februari 7, 2021 baada nafasi zote kujaa.

“Tumefunga kabisa usajili wa mbio hizo mbili lakini usajili wa Km 5 unaendelea kwa njia ya Tigo Pesa kwa kubonyeza *149*20#. Hii ni njia nyepesi ya kujisajili na tunatoa wito kwa washiriki wote wajisajili mapema kuepuka usumbufu dakika za mwisho,” walisema waandaaji hao.  

Usajili huu pia utafanyika wakati wa zoezi la uchukuaji namba za kukimbilia Jijini Dar es Salaam, Arusha na Moshi. Hata hivyo tunatoa wito kwa washiriki wote wajisajili kwa njia ya simu kuepusha usumbufu,” ilisema taarifa hiyo.
Wadhamini wa mbio za Kilimanjaro Marathon 2022 ni Kilimanjaro Premium Lager (Mdhamini Mkuu) Tigo (21km) na Grand Malt (5km).
Wadhamini wa meza za maji ni pamoja na Absa Tanzania, Unilever Tanzania, TPC Sugar, Simba Cement na Kilimanjaro Water. Wasambazaji rasmi ni GardaWorld Security, Keys Hotel, Kibo Palace Hotel, CMC Automobiles na Surveyed Plots Company Ltd (SPC) na Bodi ya Utalii (TTB).

Katika hatua nyingine, maandalizi ya maonesho yanayojulikana kama Kili Expo (The People's Expo) ambapo wadhamini na wadau wengine wa mbio hizo watapata fursa ya siku tatu za kuonyesha bidhaa na huduma wanazotoa yamekamilika.

Maonyesho hayo yanatarajiwa kufanyika kati ya Februari 24-26, 2022, katika viwanja vya MoCU na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali.
"Maonyesho haya pia linakusudiwa kuwapa uma uzoefu wa muda mrefu wa mbio za Kili Marathon; pia kwa mwaka huu wanaotarajia kushiriki mbio hizo watapata fursa ya kuchukua namba zao za ushiriki eneo la chuo kikuu cha Ushirika badala ya eneo la Keys Hotel kama ilivyokuwa miaka ya nyuma”, ilisema taarifa hiyo ya wandaaji.

Mbio za Kilimanjaro Premium Lager Marathon, zinatarajiwa kufanyika Jumapili ya Februari 27, 2022, katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), ambapo zimeandaliwa na taasisi ya Kilimanjaro Company Limited na kuratibiwa na wadau wa hapa nchini kampuni ya Executive Solutions Limited




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...