Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma ametoa wito kwa watumishi wa Mfuko kujijengea utaratibu wa kufanya mazoezi mara kwa mara kwa ajili ya kuimarisha afya zao. 

Rai hiyo imetolewa wakati wa Bonanza la WCF lililofanyika tarehe 05/02/2022 katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo watumishi wa Mfuko walishiriki.

"Michezo ina manufaa makubwa kwa afya zetu hasa katika nyakati hizi za magonjwa yasiyoambukiza hivyo tuzingatie mazoezi ili yatuweke katika hali nzuri kimwili na kiakili", alisema Dkt. Mduma.

"Michezo pia inaboresha mahusiano yetu kama watumishi pamoja na majirani zetu na wananchi kwa ujumla hivyo tuendeleze utamaduni wa kufanya mazoezi mara kwa mara", aliongeza Dkt. Mduma. 

Michezo mbalimbali ilihusika kwenye bonanza hilo la WCF ikiwemo mpira wa miguu, kuvuta kamba, jogging, riadha, kukimbiza kuku pamoja na kukimbia ndani ya magunia ambapo washindi walitunukiwa zawadi mbalimbali ikiwemo vikombe na medali.


















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...