Na.Vero Ignatus Arusha.
Ilikomesha vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na
watoto ni muhimu kuwawezesha wanawake
ili kujikwamua kiuchumi na kijamii,kwani asilimia 3% ya pato la taifa
hupotea kwasababu ya kushughulikia masuala ambayo yanaletwa na unyanyasaji wa
kijinsia
Hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongela
katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 8machi 2022 mkoani
Arusha, katika uwanja wa kumbukumbu wa shekh Ameri Abeid kwamba ukatili
utakapokomeshwa itasaidia kuokoa rasilimali fedha nyingi zinazopotezwa
kutokana
na athari za unyanyasaji na kutokuwa na usawa wa kijinsia.
‘’Mimi
naamini wanaume wenzangu sasahivi tunajihisia Amani na rah asana kuliko tunavyodhaniwa
maana yake kuna wakati wanadhani wanaume tunawasiwasi sasahivi ndio tuna amani
nafuraha kubwa zaidi kwasababu tuanajua jamii yetu ilivyo,wakina mama hawa
wakienda mbele wakawa na nguvu zaidi hata sisi maendeleo hayo yatatugusa
Naibu Waziri
wa Katiba na sheria Mhe.Geofrey Pinda Amesema kuwa kamati hizo
zikisimamiwa kama inavyotakiwa itapunguza ukatili dhidi ya wanawake na watoto
kwani umiliki wa ardhi umekuwa ni kizungumkuti kwa
wakinamama kwani hawapewi nafasi saw ana baba hivyo wizara inaendelea
kuliangalia sualahilo
Pinda amesema kuwa Maadhimisho
ya siku ya mwanamke duniani ninkutathimini na kuheshimu mchango wa
mwanamke duniani katika nyanja zote za uchumi kiutamaduni,kisiasa
kijamii katika kuleta Maendeleo katikabya kweli ukizingatia kuwa katika
tamaduni.
Pinda
amesema kuwa katika mizunguko ambayo amekuwa nikiiifanya kuzungukia mikoa kuwasikiliza wananchi matatizo ya wananchi mengi
kati yao yamekuwa suala la ndoa,mirathi na migogoro ya ardhi hivyo serikali inaendelea kulifanyia kazi
katika kulichakata.
Lipo
tatizo la mirathi ,watoto na wajane haswa wakina mama na watoto, amekuwa
wakipata matatizo na migogoro mingi, Wizara ina ndelea kuangalia
suala hili,marekebisho ya sheria ya ndoa haswa Binti
anatakiwa aolewe akiwa na umri gani,tunaendelea na mchakato pamoja na
utafsiri wa sheria.Alisema Mhe.Pinda
Kwa upande
wake Naibu katibu mkuu wa wa wizara ya maendeleo ya jamii jinsia ,wanawake na watu
wenye mahitaji maalum Amon mpanju ameiomba mikoa kuhakikisha kuwa
inaanzisha na kusimamia kamati za ulinzi wa wanawake na watoto yaani MTAKUWA
ili jamii jamii iweze kushiriki katika kupambana na vitendo vya ukatili nchini
.
Akisoma risala kwa niaba ya Wanawake kwa mgeni rasmi Upendo Laboya
alisema madhumuni ya siku hiyo ya Wanawake kujenga ushirikiano wa
wanawkae nchini,kuweka msisitizo wa Maadhimisho kwa mwaka husika,kutoa
nafasi kwa jamii kutafakari changamoto zinazowakabili wanawake na
kuzitafutia ufumbuzi,pamoja na kuelimisha Jamii kuhusu shughuli
mbalimbali za wanawake
Aidha
risala hiyo ilizidi kusema kuwa nchi ya Tanzania ipo mstari wa mbele
kwa kuwa na Mipango madhubuti ,inayoelimisha Jamii kuwa na uwiano wa
Kijinsia, katika kusimamia nakugawana rasilimali zilizopatikana katika
Jamii bila ya kuwa na upendeleo wa upande wowote.
Aidha
wamesema wanupongeza mkoa kwa kuendelea kuwahimiza wakurugenzi
,watendaji wa Halmashauri kutenga asilimia 10% katika mapato yake ya
ndani kwaajili ya mikopo kwa wanawake ,vijana,watu wenye ulemavu,kwa
uwiano wa asilimia 2 ili kutumisha Mfuko wa Maendeleo .
Katika
kuadhimisha siku hiyo wanawake mkoa wa Arusha waliweza kushiriki katika
shughuli mbalimbali ikiwemo michezo,kufanya usafili katika Kituo Cha
Afya Levolosi,kongamano,kutembelea mbuga za wanyama ambazo zimeleta
hamasa kubwa Kwa makundi yote ya wnaawake na Jamii kwa ujumla.
Aidha
Kauli mbiu hiyo inatoa nafasi na majukumu kwa kila mtu katika nafasi
yake kuapza sauti na kuchukua hatua na kutokomeza vitendo vya Ukatili
ubakaji baina ya wenza ,Ukatili wa kingono Kama vile rushwa ya
ngono,matusi ,ulawiti,kutupa au kutelekeza watoto ,ukeketaji ,Ukatili
Dhidi ya Wanawake ukiwepo Mpango wa Taifa wa kuzuia Ukatili Dhidi ya
Wanawake na watoto.
Nchini Tanzania maadhimisho ya
siku ya wanawake duniani,yamefanyika kimkoa katika uwanja wa Sheikh
Amri Abeid Jijini Arusha yakiongozwa na Kauli Mbiu ‘Kizazi cha haki na
usawa kwa maendeleo endelevu, Tujitokeze kuhesabiwa’ ambapo Mgeni Rasmi
ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...