Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) Dk.Jabiri Bakari akizingumza katika maadhimisho ya Siku ya Haki  ya Watumiaji Duniani iliyokutanisha Wanafunzi wa Vyuo Vikuu ,Sekondari pamoja na watoa huduma za mawasiliano yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.


*Yaahidi kuendelea kulea vijana na wanafunzi katika Tehama.

Na Chalila Kibuda, Michuzi TV

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema imeondoa gharama za majaribio kwa wanafunzi katika bunifu za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ili kupata matokeo chanya yatakayosaidia ukuaji wa uchumi wa kidijiti.

Pia imesema hadi kufikia Februari 2022  watumiaji wa huduma za fedha kwa njia ya simu wameongezeka na kufikia million 35.2. 

Hayo yamesemwa Jijini Dar es salaam jana na Mkurungezi Mtendaji TCRA, Dk. Jabir Bakari  wakati akifungua Maadhimisho ya Siku ya haki za watumiaji Duniani.

Alisema tayari ameshafanya mazungumzo na Kampuni zote za simu kuwa wanafunzi watakaofanya bunifu zinazohusiana hizo kupitia mtandao wasitozwe gharama yoyote na wameafikiana hivyo ili wanafunzi wa chuo na msingi kuwavutia kufanya masuala ya kitehama na kuendelea kulelewa.

"Nimeshazungumza na kampuni za simu kuwa wanafunzi wasitozwe  gharama yoyote lengo ni kupata matokeo chnya katika  uchumi wa kidigitali"amesema Dk.Bakari

Dk.Bakari alisema sekta ya mawasiliano imekuwa ikitumika kuhudumia uchumi wa fedha ambapo sasa hivi  unaweza kutumia kama benki inavyotembea ikiwemo kulipa kodi na tozo za serikali na ankala mbalimbali haya ni mafanikio katika sekta ya mawasiliano.

"Ukuaji huu umesaidia kupeleka uchumi mbele, ongezeko hilo linatoa picha kuwa watumiaji wa mtandao wa huduma za fedha wanakuwa siku hadi siku"alisema.

Alisema TCRA itaendelea kutekeleza majukumu yake kwa kulinda haki za walaji pamoja na kuandaa mazingira ili utumiaji wenye manufaa uweze kukua kwa haraka.

Naye Mkurugenzi wa Leseni na Ufuatiliaji TCRA,  John Daffa alisema TCRA walianza maadhimisho hayo kwa kuwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya oMawasiliano kwa ajili ya kutatua changamoto mbalimbal katika sekta hiyo.

Alisema maadhimisho hayo yamefanyika kwa mara ya kwanza na utaratibu huo utakuwa endelevu.

Hata hivyo maadhimisho hayo yameambatana na uzinduzi wa Klabu mbalimbli za kidigitali lengo likiwa ni kuwawezesha wanafunzi kufahamu matumizi sahihi ya mtandao.


Meneja wa kitengo kinachoshughulikia Wateja wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) Thadayo Ringo akizungumza katika  maadhimisho ya siku mtumiaji wa huduma za mawasiliano akisisitiza kizazi cha wanafunzi wa sekondari ambao ndio wanaingia katika teknolojia ya mawasiliano ,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Leseni na Ufatiliaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) John Daffa akizungumza kuhusiana na Historia ya Maadhimisho ya Haki ya Mtumiaji Duniani ambapo lengo ilikuwa ni kushirikisha wadau ambapo TCRA  inafanya hivyo ,jijini Dar es Salaam.
Afisa Uhusiano wa Halotel Stella Pius akizungumza kuhusiana umhimu wadau wa watoa huduma wa mawasiliano  katika maadhimisho ya siku ya Haki   ya Watumiaji  Duniani ,jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja ya Mkurugenzi Mkuu wa TCRA  Dk.Jabiri Bakari akiwa na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kisutu ,jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wanafunzi mbalimbali wa Sekondari wakisikiliza mada katika maadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtumiaji,Jijini Dar es Salaam.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...