Sehemu ya mizinga ya kufugua nyuki iliyopo maeneo ya Msingisi inavyoonekana.
Asali inayozalishwa na Wakala wa Huduma za Tanzania ( TFS) Wilayani Gairo ikiwa imehifadhiwa.
Mhifadhi Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Wilaya ya Gairo Robert Mwangosi ( kushoto) akifafanua jambo kuhusu Ufugaji Nyuki na faida zake.


Na Mwandishi Wetu

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)kupitia Mhifadhi Mkuu wa Wilaya ya Gairo mkoani Morogoro Robert  Mwangosi amesema wamejikita kwenye ufugaji wa nyuki kwa kuwa  wana  manzuki kubwa sana maeneo ya Msingisi ambayo  inafanya vizuri  kwenye ufugaji nyuki ambapo kwa mwaka wa fedha uliopita  wamevuna tani moja ya asali kutoka kwenye mizinga 82 tu.

Akielezea zaidi Mwangosi amesema Gairo inafanya vizuri katika suala zima la uzalishaji wa asali ,hata hivyo wamekua wakijikita katika kuwahamasisha na kuwaelimisha wananchi kuhusu  ufugaji wa nyuki.

"Asali ya Fairo inasomeka vizuri katika soko ,imekua na sifa tofauti kwani asali yetu ina sifa ya kuganda kutoka na mimea ya maeneo hayo na mimea tunayoendelea kuipanda kwani tuna mimea inayoitwa Akeshia yale maua yake ndo yanayopelekea asali hiyo kuganda,"amesema.

Pia ubora wa asali ni mzuri na hiyo imefanya asali hiyo hununuliwa na watu wa nje ya Gairo na ndo mana wanaendelea kujikita katika kuwahamasisha wananchi kupanda miti na kuangalia aina ya mimea ambayo inafanya vizuri na inayo pendwa na nyuki na kuweza kufanya vizuri katika uzalishaji wa nyuki.

Kwa upande wake Ofisa Ufugaji Nyuki TFS Gairo Aled Heneriko  ameeleza katika msimu huu wa mvua ni msimu wa nyuki kujenga hivyo ameshauri kwa wakati huu mizinga ambayo ilikua ina uchafu isafishwe ili wakati ambao makundi ya nyuki yanapokuwa yanahama kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine yaweze kuingia katika hiyo mizinga kwaajili ya kujipatia mazao mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...