Kijana ambaye hajafahamika haraka jina lake anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 mpaka 30 mkazi wa Igoma halmashauri ya mji wa Njombe amenusurika kifo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali katika mtaa wa Mpechi eneo la Lutilage mara baada ya kukamatwa akiwa ameiba vitu mbali mbali Ikiwemo TV,Godoro,Blanketi na Mtungi mdogo wa gesi.

Luo Lameck Mgeni ni mzee aliyekuwa amempangisha awali katika nyumba yake kabla ya kumfukuza kutokana na tabia ya wizi anasema anashangaa kuona kijana huyo ameondoka kwake lakini amerudi na kuiba kwenye moja ya nyumba ya familia yake.

“Leo nikasikia kule nyumbani wameboboa nikauliza wameiba nini,kuingia mle ndani tukaona tandiko halipo na vitu vingine amechana chana ameweka nje”alisema Mzee Mgeni

Hata hivyo kabla kijana huyo hajafikiwa na hali mbaya kutokana na kipigo,Polisi imefika na kufanikiwa kumuondosha katika eneo hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...