Peter Haule na Saidina Msangi, WFM, Dodoma
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb, ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Liwale kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kukamilisha taratibu za maombi ya fedha za kutekeleza mradi wa Stendi ya kisasa ya Liwale na kuwasilisha Wizara ya Fedha na Mipango.
Rai hiyo imetolewa bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Liwale, Mhe. Zuberi Mohamedi Kuchauka, aliyetaka kujua mpango wa Serikali kuirejeshea Halmashauri ya Liwale fedha za kutekeleza miradi ya kimkakati ilizozirejesha Hazina.
“Halmashauri ya Wilaya ya Liwale imetengewa shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa stendi hiyo katika mwaka 2021/22, nia ya Serikali ni kuhakikisha kuwa mradi huo unatekelezwa kutokana na umuhimu wake”, alieleza Mhe. Chande.
Alisema kuwa ujenzi wa stendi ya Kisasa ya Liwale mkoani Lindi ni moja kati ya miradi ya kimkakati ya kuongeza mapato kwa Halmashauri ambapo mwaka 2018 Serikali iliingia mkataba na Halmashauri ya Liwale kutekeleza mradi huo kwa gharama ya shilingi bilioni 1.2.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...