
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango leo amemuwakilisha Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika Mazishi ya kitaifa ya aliyekuwa Rais wa Tatu wa Jamhuri ya Kenya ,Hayati Emilio Mwai Kibaki. Ibada ya kumuaga Hayati Mwai Kibaki imefanyika katika Uwanja wa Nyayo uliopo Nairobi nchini Kenya na kuongozwa na Rais wa Jamhuri ya Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta.
Viongozi Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka mataifa mbalimbali, wawakilishi wa taasisi za kitaifa na kimataifa pamoja na mabalozi, wananchi wa Kenya na nchi jirani wamehudhuria kuagwa kwa Hayati Mwai Kibaki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...